Friday, May 20, 2022
27 °c
Dar es Salaam
25 ° Thu
25 ° Fri
25 ° Sat
25 ° Sun
25 ° Mon
English EN Kiswahili SW
UHURU MEDIA GROUP
Tangaza Nasi
  • Mwanzo
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHAKA ANG’AKA FAINI MIMBA ZA WANAFUNZI

    NI HISTORIA NYINGINE CCM

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM YATEUA MAKATIBU WA MIKOA NA WILAYA

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM ITAENDELEA KUWA CHAMA BORA, IMARA AFRIKA- SHAKA

    MBISE ATOA VITI MIA MOJA MONDULI

    MBISE ATOA VITI MIA MOJA MONDULI

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
  • Michezo
    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    PABLO AIPANIA KMC 

    PABLO AIPANIA KMC 

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
  • UMG
    • Home
    • About Us
    • Services
    • Shop
    • Contact Us
  • MAGAZETI
    • Uhuru wanawake
    • Mzalendo
    • Uhuru vijijini
    • Burudani
    • Uhuru kijani
  • UHURU FM
    • Ratiba
  • UHURU DIGITAL
    • Instagram
    • Facebook
    • Twitter
    • Youtube
  • Mwanzo
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHAKA ANG’AKA FAINI MIMBA ZA WANAFUNZI

    NI HISTORIA NYINGINE CCM

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM YATEUA MAKATIBU WA MIKOA NA WILAYA

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM ITAENDELEA KUWA CHAMA BORA, IMARA AFRIKA- SHAKA

    MBISE ATOA VITI MIA MOJA MONDULI

    MBISE ATOA VITI MIA MOJA MONDULI

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
  • Michezo
    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    PABLO AIPANIA KMC 

    PABLO AIPANIA KMC 

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
No Result
View All Result
UHURU MEDIA GROUP
No Result
View All Result
Mwanzo Habari Kitaifa

CCM YAPONGEZA MAONO YA SAMIA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 2, 2021
in Habari Kitaifa
0 0
0
CCM YAPONGEZA MAONO YA SAMIA

KATIBU wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Itikadi na Uenezi, Shaka Hamdu Shaka

0
SHARES
77
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimesifu hatua ya Rais Samia Suluhu Hassan, kujali na kuwasilikiza wananchi kwa kushughulikia malalamiko yaliyotokana na tozo za miamala ya simu, kikimtaja kuwa na msimamo imara na thabiti.

Kimesema punguzo la tozo hizo ni unafuu kwa wananchi, ambao idadi kubwa wamekuwa wakitumia miamala ya simu kuendesha shughuli za kiuchumi na kusaidia wahitaji.

Kauli hiyo imetolewa jijini Dar es Salaam na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Itikadi na Uenezi, Shaka Hamdu Shaka, wakati akizungumza na vijana wa taasisi ya mama yangu, nchi yangu inayoshughulika na uhamasishaji vijana.

Shaka alisema uamuzi huo umetolewa wakati mwafaka na kusisitiza kuwa pamoja na punguzo hilo, wananchi wanapaswa kufahamu wana wajibu wa moja kwa moja kuchangia maendeleo ya ujenzi wa taifa. Shaka alisema kitendo kilichofanywa na serikali chini ya Rais Samia, kimeonyesha uzalendo na uungwana kwa kuwajali na kuwasikiliza wananchi wake.

“CCM inampongeza Rais Samia kuwasikiliza wananchi kuhusu sakata la tozo za miamala ya simu, ambapo alitoa maelekezo ya viwango hivyo kutazamwa upya na sasa imepunguzwa kwa asilimia 30 huku kampuni zikipunguza kwa asilimia 10.

“Kazi ya kujenga nchi ni wajibu wa Watanzania wote bila kujali itikadi za kisiasa. Uamuzi huu ni upendo mkubwa alionao kwa wananchi anaowaongoza ili washiriki kuchangia maendeleo ya nchi yao kwa furaha,” alisema Shaka.

Hata hivyo, alibainisha wananchi wanapaswa kuelewa ni jukumu la kila mmoja kushiriki kazi ya ujenzi wa nchi na kuweka msukumo wa maendeleo na kupeleka huduma za jamii katika maeneo yote.

Aliwataka watendaji wa serikali kutambua kuwa kazi ya kumsadia Rais Samia katika kila eneo ni wajibu usiohitaji kuelelezwa wala kusukumwa, badala yake wautimize ipasavyo wakiweka mbele maslahi ya umma.

Shaka aliwataka Watanzania kupuuza uvumi unaoenezwa mitaani kuwa serikali ina mpango wa kusitisha elimu bila ada.

“Serikali ya Rais Samia itaendelea kugharamia elimu bila ada kwani unawagusa na kuwanufaisha wananchi walio wengi.

Zaidi itaendelea kutatua changamoto zilizokuwa zikikabili mpango huu ili wanafunzi wa Tanzania wapate elimu katika mazingira mazuri zaidi. Hivyo niwaombe wananchi wapuuze taarifa zinazodai serikali itausitisha,” alisema.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kundi hilo, Agness Maganga, alieleza kuwa wanamuunga mkono Rais Samia kwa kuwa serikali anayoiongoza imefanya mambo makubwa yakiwemo kupandisha madaraja watumishi wa umma 92000.

Pia kuondoa tozo ya asilimia sita ya kulinda thamani ya mkopo kwa wanufaika wa mkopo elimu ya juu, kuongeza bajeti ya mikopo elimu ya juu na kuendelea kutoa fedha kukamilisha na kuendeleza miradi mikubwa ya kimkakati nchini.

KATIBU wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Itikadi na Uenezi, Shaka Hamdu Shaka, akizungumza na vijana wa taasisi inayoshughulika na uhamasishaji vijana ya Mama Yangu, Nchi Yangu, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba Dar es Salaam.

KAULI ZA WATOA HUDUMA ZA SIMU

Akizungumza na UHURU, Mwenyekiti wa Chama cha Watoa Huduma za Mitandao ya Simu Tanzania (TAMNOA), Hisham Hendi, alipongeza hatua ya serikali kufanya mazungumzo nao kujadili mbinu za haraka na muda mrefu katika ufanikishwaji wa azma ya serikali ya kuanzisha tozo ya mshikamano.

“Tunaipongeza serikali kupitia Wizara ya Fedha na Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, kufanya mazungumzo kadhaa na tasnia hii kujadili mbinu za haraka na za muda mrefu ili kufanikisha azma ya serikali kuanzisha tozo ya mshikamano na kujadili kwa upana ustawi wa sekta hii,” alisema.

Pia aliipongeza serikali kupunguza asilimia 30 ya tozo hiyo, huku wao wakiwa wamepunguza asilimia 10 na kuongeza kuwa, ni imani yao kuwa hatua hiyo zitarudisha wateja walioacha kutumia huduma hiyo au kufanya biashara.

Hendi ambaye pia ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Vodacom, alibainisha kuwa katika katika enzi ya 4IR, sekta ya mawasiliano ina jukumu la kuziwezesha nyingine, zikiwemo ‘agritech’, ‘telemedicine’, malipo ya serikali na huduma katika kuendelea kuchangia ukuaji wa Taifa.

“Wanachama wa TAMNOA wamejitolea kuendelea kuwekeza katika ubunifu na uvumbuzi mpya lakini ili kufikia huko ni muhimu tuendelee kupata faida,” alisema.

Alisisitiza kuwa, ni muhimu kwa wadau wa sekta hiyo kufanya kazi kwa karibu na serikali, ili kujengeana maarifa juu ya ukusanyaji ushuru kupitia majukwaa ya kidigitali yanayofanya kazi kwa karibu na wadhibiti na wadau wengine kuhakikisha kufikiwa kwa malengo kwa usawa kati ya sekta binafsi na umma.

Na JUMA ISSIHAKA

 

Abdurahman Jumanne

Abdurahman Jumanne

Stay Connected test

  • 111 Follower
  • 168k Subscriber
  • 23.5k Follower
  • 99 Subscriber
  • Trending
  • Comments
  • Latest
MADAKTARI WAELEZEA JINSI YA KUZUIA MIMBA ISIHARIBIKE

MADAKTARI WAELEZEA JINSI YA KUZUIA MIMBA ISIHARIBIKE

July 9, 2021
TABWA YAMSIFU SAMIA KUWAPA FURSA WANAWAKE

TABWA YAMSIFU SAMIA KUWAPA FURSA WANAWAKE

July 9, 2021
BEI MPYA YA MBAAZI, KUNDE YAWAPANDISHA MZUKA WAKULIMA

BEI MPYA YA MBAAZI, KUNDE YAWAPANDISHA MZUKA WAKULIMA

August 9, 2021
MBUNGE LINDI ATAKA VIJANA WAJISHUGHULISHE

MBUNGE LINDI ATAKA VIJANA WAJISHUGHULISHE

July 8, 2021
DK. MWINYI ASISITIZA UIMARA WA UCHUMI

DK. MWINYI ASISITIZA UIMARA WA UCHUMI

0
MAJALIWA AANIKA SIRI UJENZI VYUO VYA VETA

MAJALIWA AANIKA SIRI UJENZI VYUO VYA VETA

0
RAIS MUSEVENI AKAMILISHA ZIARA YAKE NCHINI

RAIS MUSEVENI AKAMILISHA ZIARA YAKE NCHINI

0
USWISI KUENDELEA KUIMARISHA UHUSIANO TANZANIA

USWISI KUENDELEA KUIMARISHA UHUSIANO TANZANIA

0
TAKUKURU YAIVALIA NJUGA MIRADI ILIYOKATALIWA MBIO ZA MWENGE

TAKUKURU YAIVALIA NJUGA MIRADI ILIYOKATALIWA MBIO ZA MWENGE

May 18, 2022
VIKUNDI VILIVYOPATA MIKOPO YA BILIONI 4/- VYAITWA TAKUKURU

VIKUNDI VILIVYOPATA MIKOPO YA BILIONI 4/- VYAITWA TAKUKURU

May 18, 2022
SHAKA AZIAGIZA WIZARA TATU MISITU YA HIFADHI

SHAKA AZITAKA TAASISI ZA UMMA NCHINI KUTENGA BAJETI ZA MIRADI

May 18, 2022
WIZARA YAANIKA MKAKATI MPYA KUKABILI BEI YA MBOLEA, MAFUTA

WIZARA YAANIKA MKAKATI MPYA KUKABILI BEI YA MBOLEA, MAFUTA

May 18, 2022

Recent News

TAKUKURU YAIVALIA NJUGA MIRADI ILIYOKATALIWA MBIO ZA MWENGE

TAKUKURU YAIVALIA NJUGA MIRADI ILIYOKATALIWA MBIO ZA MWENGE

May 18, 2022
VIKUNDI VILIVYOPATA MIKOPO YA BILIONI 4/- VYAITWA TAKUKURU

VIKUNDI VILIVYOPATA MIKOPO YA BILIONI 4/- VYAITWA TAKUKURU

May 18, 2022
SHAKA AZIAGIZA WIZARA TATU MISITU YA HIFADHI

SHAKA AZITAKA TAASISI ZA UMMA NCHINI KUTENGA BAJETI ZA MIRADI

May 18, 2022
WIZARA YAANIKA MKAKATI MPYA KUKABILI BEI YA MBOLEA, MAFUTA

WIZARA YAANIKA MKAKATI MPYA KUKABILI BEI YA MBOLEA, MAFUTA

May 18, 2022
Instagram Youtube Twitter VK Facebook

We are a diverse team of experts, innovative thinkers, creative designers, writers, innovators, strategists, pyschologists, comunictaors and web developers. UMG is extremely passionate about growing clients’ businesses, helping them achieve their goals and making a difference by raising the creative and communications industry standards in Tanzania.

Follow Us

Browse by Category

  • 2021
  • Afya Makala
  • BURUDANI
  • Business
  • GAZETI LA BURUDANI
  • GAZETI LA UHURU
  • GAZETI LA UHURU MACHI 17
  • HABARI KIMATAIFA
  • Habari Kitaifa
  • Habari Picha
  • KIMATAIFA
  • MAKALA
  • MAKALA AFYA
  • MAKALA-BURUDANI
  • MICHEZO
  • MICHEZO KIMATAIFA
  • MICHEZO KITAIFA
  • MICHEZO-MAKALA
  • MICHEZO-MASUMBWI
  • MITINDO
  • RIWAYA
  • SIASA
  • Uncategorized

Recent News

TAKUKURU YAIVALIA NJUGA MIRADI ILIYOKATALIWA MBIO ZA MWENGE

TAKUKURU YAIVALIA NJUGA MIRADI ILIYOKATALIWA MBIO ZA MWENGE

May 18, 2022
VIKUNDI VILIVYOPATA MIKOPO YA BILIONI 4/- VYAITWA TAKUKURU

VIKUNDI VILIVYOPATA MIKOPO YA BILIONI 4/- VYAITWA TAKUKURU

May 18, 2022

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

No Result
View All Result

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In