Saturday, May 21, 2022
27 °c
Dar es Salaam
25 ° Thu
25 ° Fri
25 ° Sat
25 ° Sun
25 ° Mon
English EN Kiswahili SW
UHURU MEDIA GROUP
Tangaza Nasi
  • Mwanzo
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHAKA ANG’AKA FAINI MIMBA ZA WANAFUNZI

    NI HISTORIA NYINGINE CCM

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM YATEUA MAKATIBU WA MIKOA NA WILAYA

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM ITAENDELEA KUWA CHAMA BORA, IMARA AFRIKA- SHAKA

    MBISE ATOA VITI MIA MOJA MONDULI

    MBISE ATOA VITI MIA MOJA MONDULI

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
  • Michezo
    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    PABLO AIPANIA KMC 

    PABLO AIPANIA KMC 

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
  • UMG
    • Home
    • About Us
    • Services
    • Shop
    • Contact Us
  • MAGAZETI
    • Uhuru wanawake
    • Mzalendo
    • Uhuru vijijini
    • Burudani
    • Uhuru kijani
  • UHURU FM
    • Ratiba
  • UHURU DIGITAL
    • Instagram
    • Facebook
    • Twitter
    • Youtube
  • Mwanzo
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHAKA ANG’AKA FAINI MIMBA ZA WANAFUNZI

    NI HISTORIA NYINGINE CCM

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM YATEUA MAKATIBU WA MIKOA NA WILAYA

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM ITAENDELEA KUWA CHAMA BORA, IMARA AFRIKA- SHAKA

    MBISE ATOA VITI MIA MOJA MONDULI

    MBISE ATOA VITI MIA MOJA MONDULI

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
  • Michezo
    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    PABLO AIPANIA KMC 

    PABLO AIPANIA KMC 

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
No Result
View All Result
UHURU MEDIA GROUP
No Result
View All Result
Mwanzo Habari Kitaifa

DK. MWINYI ATOA MAAGIZO MATATU SIKU YA SHERIA

MAELEKEZO>>>Kuwepo sheria na mifumo ya utoaji haki itakayovutia wawekezaji 

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
February 8, 2022
in Habari Kitaifa
0 0
0
DK. MWINYI ATOA MAAGIZO MATATU SIKU YA SHERIA

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi,

0
SHARES
44
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema wakati umefika Zanzibar kuanzisha kituo cha utatuzi wa migogoro ya kibiashara.                                                                                                                                                                                                       

Amesema lengo la kufanya hivyo ni kwenda sambamba na hatua ya serikali ya kuvutia wawekezaji katika miradi mikubwa.

Dk. Mwinyi aliyasema hayo, katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Sheria Zanzibar, hafla iliyofanyika ukumbi wa Sheikh Idrissa Abdul-wakil, Kikwajuni, Jijini Zanzibar.

“Nadhani tunalazimika sasa kutunga sheria ya utatuzi wa migogoro ya kibiashara, ili tukishaipata tuwe na chombo au kuanzisha kituo cha utatuzi wa migogoro ya kibiashara hapa Zanzibar,” alisema.

Dk. Mwinyi alisema amezingumza na Mwanasheria wa Serikali, hivyo ni matumaini yake miradi mikubwa inayofanyika Zanzibar migogoro yake haitapelekwa mahakamani.

“Hakuna sababu ya hilo, kwa kuwa Nairobi wamefanya, Kigali wamefanya na sioni kwanini Zanzibar tusifanye jambo hilo,” alisema na kusisitiza ni vyema kuwepo kwa sheria na mifumo ya utoaji haki itakayovutia wawekezaji  na kuweka vitega uchumi vyao nchini na kutoa ajira kwa wananchi.

USIMAMIZI WA UTOAJI WA HAKI

Dk. Mwinyi alieleza kuwa ni muhimu viongozi katika sekta zote kuzingatia na kusimamia vizuri utoaji wa haki, ili imani ya wananchi kwa serikali na vingozi iongezeke.

Alisisitiza utoaji wa haki kwa misingi ya sheria na usawa inaepusha jamii na migogoro isiyokuwa na lazima na inawahamasisha wananchi kushiriki kikamilifu shughuli za maendeleo.

“Kwa kutambua hali hiyo, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea kuboresha taasisi na mifumo ya utoaji wa haki, ili kuimarisha kasi ya maendeleo na ujenzi wa nchi,” aliahidi.

Pia, aliwataka wataalamu wa sheria katika sekta ya umma na binafsi, kujiendeleza kitaaluma na kushiriki katika mafunzo mbalimbali hususan maeneo mapya ya sheria yanayohitajika kutekeleza mageuzi ya kiuchumi yanayopangwa.

Alisema utaalamu wa sheria lazima uwe katika maeneo yote ili kukidhi mahitaji ya wawekezaji na washiriki wa maendeleo waliopo nchini.

Aliongeza kwamba mifumo ya sheria iliyopo ni lazima iwe chachu ya kuwaondolea wananchi ugumu wa maisha na kuwawezesha kujiajiri wenyewe kwa lengo la kuchangia maendeleo ya nchi.

Alisema siyo jambo linalopendeza kwa wananchi na wawekezaji kuchukua muda mrefu mahakamani na katika taasisi nyingine za utoaji wa haki.

Dk. Mwinyi alieleza kumekuwepo malalamiko mengi yanayowasilishwa kwake kupitia  Mtandao wa Sema na Rais, kuhusu ucheleweshaji wa utoaji haki unaofanywa na baadhi ya viongozi wa taasisi za serikali, hivyo aliwahimiza viongozi kuongeza bidii katika usimamizi wa haki za wananchi kwa kuzingatia sheria.

Rais Dk. Mwinyi alisema serikali inaendelea kuchukua hatua mbalimbali katika kuimarisha mazingira ya utoaji wa haki, ikiwemo kufanikisha ujenzi wa  majengo ya kisasa ya taasisi hizo na kuzipatia nyenzo kwa kadri hali ya fedha na uchumi inavyoruhusu.

USHIRIKIANO MAHAKAMA YA ZANZIBAR NA TANZANIA

Dk. Mwinyi alisisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano kati ya Mahakama ya Tanzania, Mahakama ya Zanzibar  na taasisi zote za utoahji haki nchini na kubainisha maeneo mbalimbali ya ushirikiano.

Maeneo hayo ni matumizi ya lugha ya Kiswahili, mifumo ya TEHAMA, mafunzo kwa watumishi, namna bora ya kupambana na dawa za kulevya na usuluhishi wa migogoro.

Dk. Mwinyi alimpongeza Kaimu Jaji Mkuu wa Zanzibar Khamis Rmadhan Abdalla kwa kuleta mabadiliko makubwa ya kiutendaji katika kipindi kifupi, na hivyo akawataka watendaji na watumishi wa mhimili huo kuunga mkono juhudi hizo.

Aliushukuru uongzi wa Mahakama ya Tanzania kupitia Jaji Mkuu, Jaji Kiongozi na Mtendaji Mkuu wa Mahakama kuanza kuisaidia Mahakama ya Zanzibar.

MATUMIZI YA LUGHA YA KISWAHILI MAHAKAMANI

Dk. Mwinyi alihimiza utumiaji wa lugha ya Kiswahili katika Mahakama za Zanzibar, ili kuwasaidia wananchi kutopoteza haki zao kwa kutokuelewa lugha ya Kiingereza inayotumika.

Alisema lugha ni nyenzo muhimu katika usimamizi wa haki, ambapo upo uwezekano mkubwa watu kupoteza haki zao kwa sababu ya kutoelewa lugha ya kigeni inayotumika.

“Tuhakikishe uendeshaji wa mashauri na uandishi wa sheria unafanywa zaidi kwa lugha ya kiswahili badala ya lugha ya kigeni,” alisema.

KAIMU JAJI MKUU ZANZIBAR

Awali, Kaimu Jaji Mkuu wa Zanzibar Khamis Ramadhan Abdalla alisema kauli mbiu ya maadhimisho hayo isemayo ‘Usimamizi wa Haki ni Msingi wa Maendeleo ya Kiuchumi na Kijamii”, imezingatia  hatua zinazoendelea kuchukuliwa na serikali katika kujenga Uchumi wa Buluu.

Alisema pamoja na mafanikio yaliyopatikana katika utekelezaji wa dhana hiyo, kumekuwa na mwamko mdogo kwa wafanyabaishara wa Zanzibar kufungua kesi katika Mahakama ya Biashara.

Alisema katika mwaka 2021 kulikuwa na mashauri 11 pekee yalioripotiwa mahakamani, hivyo akatoa ahadi ya kuendeleea kuitangaza Mahakama hiyo kwa jamii ili itumike kikamilifu.

Aliyataja  miongoni mwa mafanikio yaliyopatikana katika usimamizi wa haki ni kuwepo kwa mahakimu sita wanaosikiliza kesi za udhalilishaji na Mahakimu watatu wa kusikiliza kesi za dawa za kulevya.

Alisema kwa mujibu wa utaratibu Mahakimu hao hawapangiwi kesi za aina nyingine, huku muda wa kusikiliza kesi ukiongezwa hadi saa 11, ikiwa ni hatua ya kumaliza mashauri hayo kwa haraka na kutoa fursa kwa wananachi kufanya kazi nyengine.

Kuhusu ongezeko la mahabusu katika Magereza Kisiwani Pemba, Kaimu Jaji Mkuu alisema amewaagiza Mahakimu kutoa dhamana kwa mahabusu wa kesi zote zenye dhamana na kuongeza nguvu ya usikilizaji kwa kesi ambazo hazina dhamana, huku  Mahakama ikizingatia mfumo wa kutekeleza adhabu katika jamii.

Jaji Khamis alitoa wito kwa jamii kuondokana na tabia iliyojitokeza ya uwepo wa ushirikiano kwa lengo la kuharibu kesi hususan za udhalilishaji kwa wadhuriwa  wenye umri wa kuanzia miaka 15  hadi miaka 17.

WAZIRI WA KATIBA

Naye, Waziri wa  Nchi, Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria , Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Haroun Ali Suleiman alisema kuna mabadiliko ya kiutendaji katika shughuli za kimahakama na kubainisha kuwepo ushirikiano mkubwa kwa watendaji wa usimamizi wa haki, ikiwemo Ofisi ya Mwendesha Mashtaka, Jeshi la  Polisi, Mahakama na Mawakili.

Aidha, Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Dk. Mwinyi  Talib Haji alisisitiza umuhimu wa dhana ya Uchumi wa Buluu  kuzungumzwa mara kwa mara.

Mkurugenzi wa Mashitaka Zanzibar, Salma Ali Khamis alisema changamoto kubwa inayokwaza utekelezaji wa usimamizi wa haki ni ile ya wananchi kushindwa kufika Mahakamani kutoa ushahidi hususan katika kesi za udhalilishaji, hivyo akabinisha umuhimu wa  kuwepo mabadiliko ya kiutendaji na kisera.

Rais wa Chama cha Mawakili Zanzibar, Dk. Slim Abdalla aliishauri serikali kuweka mkazo katika utatuzi wa migogoro ya kiuchumi, kifedha na kibiashara na kusisitiza umuhimu wa Zanzibar kuanzisha kituo cha utatuzi wa migogoro ya kibiashara.

Siku ya Sheria Zanzibar huadhimishwa kila ifikapo Februari 2 kila mwaka, ikiashiria kuanza kwa mwaka mpya wa Mahakama.

NA HANIFA RAMADHANI, ZANZIBAR

Abdurahman Jumanne

Abdurahman Jumanne

Stay Connected test

  • 111 Follower
  • 168k Subscriber
  • 23.5k Follower
  • 99 Subscriber
  • Trending
  • Comments
  • Latest
MADAKTARI WAELEZEA JINSI YA KUZUIA MIMBA ISIHARIBIKE

MADAKTARI WAELEZEA JINSI YA KUZUIA MIMBA ISIHARIBIKE

July 9, 2021
TABWA YAMSIFU SAMIA KUWAPA FURSA WANAWAKE

TABWA YAMSIFU SAMIA KUWAPA FURSA WANAWAKE

July 9, 2021
BEI MPYA YA MBAAZI, KUNDE YAWAPANDISHA MZUKA WAKULIMA

BEI MPYA YA MBAAZI, KUNDE YAWAPANDISHA MZUKA WAKULIMA

August 9, 2021
MBUNGE LINDI ATAKA VIJANA WAJISHUGHULISHE

MBUNGE LINDI ATAKA VIJANA WAJISHUGHULISHE

July 8, 2021
JAFO AWATAKA WAKAZI WA MKOA WA MARA KUJIKITA KATIKA ZAO LA ALIZETI

JAFO AWATAKA WAKAZI WA MKOA WA MARA KUJIKITA KATIKA ZAO LA ALIZETI

0
KIHONGOSI : NGORONGORO MCHAGUENI SHANGAI

KIHONGOSI : NGORONGORO MCHAGUENI SHANGAI

0
JWTZ IKO IMARA KUKABILI MATUKIO YA KIGAIDI-SERIKALI

JWTZ IKO IMARA KUKABILI MATUKIO YA KIGAIDI-SERIKALI

0
MAJALIWA AANIKA SIRI UJENZI VYUO VYA VETA

MAJALIWA AANIKA SIRI UJENZI VYUO VYA VETA

0
MIPAKA YA TANZANIA IPO SHWARI

MIPAKA YA TANZANIA IPO SHWARI

May 20, 2022
SERIKALI YATOA KIPAUMBELE CHA AJIRA KWA WENYE ULEMAVU

SERIKALI YATOA KIPAUMBELE CHA AJIRA KWA WENYE ULEMAVU

May 20, 2022
RAIS SAMIA: MAWAZIRI CHAPENI KAZI, MSISIKILIZE MANENO

RAIS SAMIA: MAWAZIRI CHAPENI KAZI, MSISIKILIZE MANENO

May 20, 2022
TAKUKURU YAIVALIA NJUGA MIRADI ILIYOKATALIWA MBIO ZA MWENGE

TAKUKURU YAIVALIA NJUGA MIRADI ILIYOKATALIWA MBIO ZA MWENGE

May 18, 2022

Recent News

MIPAKA YA TANZANIA IPO SHWARI

MIPAKA YA TANZANIA IPO SHWARI

May 20, 2022
SERIKALI YATOA KIPAUMBELE CHA AJIRA KWA WENYE ULEMAVU

SERIKALI YATOA KIPAUMBELE CHA AJIRA KWA WENYE ULEMAVU

May 20, 2022
RAIS SAMIA: MAWAZIRI CHAPENI KAZI, MSISIKILIZE MANENO

RAIS SAMIA: MAWAZIRI CHAPENI KAZI, MSISIKILIZE MANENO

May 20, 2022
TAKUKURU YAIVALIA NJUGA MIRADI ILIYOKATALIWA MBIO ZA MWENGE

TAKUKURU YAIVALIA NJUGA MIRADI ILIYOKATALIWA MBIO ZA MWENGE

May 18, 2022
Instagram Youtube Twitter VK Facebook

We are a diverse team of experts, innovative thinkers, creative designers, writers, innovators, strategists, pyschologists, comunictaors and web developers. UMG is extremely passionate about growing clients’ businesses, helping them achieve their goals and making a difference by raising the creative and communications industry standards in Tanzania.

Follow Us

Browse by Category

  • 2021
  • Afya Makala
  • BURUDANI
  • Business
  • GAZETI LA BURUDANI
  • GAZETI LA UHURU
  • GAZETI LA UHURU MACHI 17
  • HABARI KIMATAIFA
  • Habari Kitaifa
  • Habari Picha
  • KIMATAIFA
  • MAKALA
  • MAKALA AFYA
  • MAKALA-BURUDANI
  • MICHEZO
  • MICHEZO KIMATAIFA
  • MICHEZO KITAIFA
  • MICHEZO-MAKALA
  • MICHEZO-MASUMBWI
  • MITINDO
  • RIWAYA
  • SIASA
  • Uncategorized

Recent News

MIPAKA YA TANZANIA IPO SHWARI

MIPAKA YA TANZANIA IPO SHWARI

May 20, 2022
SERIKALI YATOA KIPAUMBELE CHA AJIRA KWA WENYE ULEMAVU

SERIKALI YATOA KIPAUMBELE CHA AJIRA KWA WENYE ULEMAVU

May 20, 2022

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

No Result
View All Result

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In