Saturday, August 13, 2022
27 °c
Dar es Salaam
25 ° Thu
25 ° Fri
25 ° Sat
25 ° Sun
25 ° Mon
English EN Kiswahili SW
UHURU MEDIA GROUP
Tangaza Nasi
  • Mwanzo
  • Siasa
    • All
    • Business
    MEMBE ATOA YA MOYONI AKIREJEA CCM

    MEMBE ATOA YA MOYONI AKIREJEA CCM

    SHAKA ANG’AKA FAINI MIMBA ZA WANAFUNZI

    NI HISTORIA NYINGINE CCM

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM YATEUA MAKATIBU WA MIKOA NA WILAYA

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM ITAENDELEA KUWA CHAMA BORA, IMARA AFRIKA- SHAKA

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
  • Michezo
    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    PABLO AIPANIA KMC 

    PABLO AIPANIA KMC 

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
  • UMG
    • Home
    • About Us
    • Services
    • Shop
    • Contact Us
  • MAGAZETI
    • Uhuru wanawake
    • Mzalendo
    • Uhuru vijijini
    • Burudani
    • Uhuru kijani
  • UHURU FM
    • Ratiba
  • UHURU DIGITAL
    • Instagram
    • Facebook
    • Twitter
    • Youtube
  • Mwanzo
  • Siasa
    • All
    • Business
    MEMBE ATOA YA MOYONI AKIREJEA CCM

    MEMBE ATOA YA MOYONI AKIREJEA CCM

    SHAKA ANG’AKA FAINI MIMBA ZA WANAFUNZI

    NI HISTORIA NYINGINE CCM

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM YATEUA MAKATIBU WA MIKOA NA WILAYA

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM ITAENDELEA KUWA CHAMA BORA, IMARA AFRIKA- SHAKA

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
  • Michezo
    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    PABLO AIPANIA KMC 

    PABLO AIPANIA KMC 

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
No Result
View All Result
UHURU MEDIA GROUP
No Result
View All Result
Mwanzo Habari Kitaifa

HOSPITALI MAALUMU YA MAMA NA MTOTO KUJENGWA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
May 17, 2022
in Habari Kitaifa
0 0
0
HOSPITALI MAALUMU YA MAMA NA MTOTO KUJENGWA

WAZIRI wa Afya, Ummy Mwalimu

0
SHARES
70
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

SERIKALI chini ya Rais Samia Suluhu Hassan Imetenga kiasi cha sh trilioni 1.1 kwa Wizara ya Afya kwa mwaka wa fedha 2022/2023.

Fedha hizo zitatumika kutekeleza vipaumbele 16 vya afya, ambapo kwa mara ya kwanza Tanzania itakuwa na Hospitali Maalumu ya Mama na Mtoto.

Katika fedha hizo, Serikali inatarajia kutumia sh. bilioni 200 kwa ajili ya ununuzi wa dawa, vifaa, vifaa tiba na vitendanishi kisha kusambazwa katika ngazi zote za utoaji wa huduma za afya.

Akiwasilisha bungeni, hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Afya kwa mwaka wa fedha 2022/2023, Waziri wa wizara hiyo, Ummy Mwalimu, amesema wizara itaendelea kubuni na kutekeleza mikakati mbalimbali kuhakikisha huduma za afya nchini zinawafikia Watanzania walio wengi hususan wenye kipato cha chini.

“Kipekee nimpongeze Rais Samia kwa uongozi wake imara na kwa dhamira, maono na uthubutu wake, ambao umekuwa dira sahihi inayoongoza utendaji wangu katika kuimarisha utoaji wa huduma za afya nchini.

“Ni dhahiri katika kipindi cha uongozi wake Watanzania wameshuhudia kasi kubwa ya uimarishaji na utoaji wa huduma bora za afya nchini, hususan ujenzi na uboreshaji wa miundombinu ya afya katika halmashauri na mikoa yote nchini, kuimarisha upatikanaji wa dawa, vifaa, vifaa tiba na huduma za matibabu ya kibingwa na ubingwa bobezi katika hospitali za rufani za mikoa, kanda na Taifa,” alieleza.

 VIPAUMBELE 16 VYA WIZARA

Ummy ambaye pia ni Mbunge wa Tanga Mjini (CCM) alisema ili kutekeleza vipaumbele vilivyoanishwa katika mwaka wa fedha 2022/2023, wizara imekadiria kutumia kiasi cha sh. trilioni 1.1 kutekeleza majukumu yake ya uendeshaji wa ofisi na miradi wa maendeleo.

Alisema wizara imepanga kununua, kutunza, kusambaza na kutoa chanjo kwa watoto nchini, ambapo sh. bilioni 74.4 zimetengwa na kujenga hospitali maalumu ya Mama na Mtoto jijini Dodoma kuimarisha huduma za tiba kwa magonjwa ya wanawake na watoto ambapo sh. bilioni 10 kimetengwa.

Waziri Ummy alisema sh. bilioni 23.36 kimetengwa kwa ajili ya kujenga vyumba vya huduma za watoto wachanga katika hospitali 100 za wilaya, kuwajengea uwezo watoa huduma kuwa na stadi, weledi, tabia bora katika kutoa huduma za mama na mtoto, kujenga, kuweka vifaa na watumishi wenye weledi katika wodi za wagonjwa wanaohitajai uangalizi maalumu (ICU) za wazazi katika hospitali za kanda na mikoa.

Alitaja kipaumbele cha tatu ni kununua dawa, vifaa, vifaa tiba na vitendanishi na kuzisambaza katika ngazi zote za utoaji wa huduma za afya, serikali imetenga sh. bilioni 200, kazi ya ukamilishaji ujenzi wa hospitali tano za rufani za mikoa ya Katavi, Geita, Njombe, Songwe na Simiyu, zimetengwa sh. bilioni 18.6.

“Eneo lingine ni kukamilisha ujenzi wa hospitali mpya tatu za rufani za mikoa ya Shinyanga, Singida na Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (Mara) ambapo sh. bilioni 26 zimetengwa.

Kuboresha huduma za matibabu ya ubingwa bobezi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili na za kanda kwa kuimarisha miundombinu na ununuzi wa vifaa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), hospitali za rufani za kanda za Chato, Mtwara, KCMC, Bugando, Mbeya na kuanza ujenzi wa Hospitali ya Rufani ya Kanda ya Magharibi, uimarishaji wa Hospitali Teule ya Ukerewe zimetengwa sh. bilioni 16.9

Aliongeza kuwa: “Kuendelea na ujenzi wa wodi ya wagonjwa binafsi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili zimetengwa sh. bilioni nne, kuanza ujenzi wa jengo la kutolea huduma za uchunguzi na tiba ya saratani, ikiwemo huduma ya mionzi katika Hospitali ya Benjamini Mkapa Dodoma ambapo zimetengwa sh. bilioni 10.”

Ummy alikitaja kipaumbele cha kingine ni kukamilisha upanuzi wa miundombinu ya kutolea huduma za afya katika hospitali nane za rufani za mikoa ambayo mikataba yake bado inaendelea.

Alizitaja hospitali hizo kuwa ni Ligula (Mtwara) Tumbi (Pwani), Bombo (Tanga), Kagera, Maweni (Kigoma), Kitete (Tabora), Sekou – Toure (Mwanza) na Mawenzi (Kilimanjaro) ambapo zimetengwa sh. bilioni 13.6.

Waziri huyo alitaja kipaumbele cha 10 ni kuendelea na ujenzi wa hospitali mbili mpya za mikoa ya Ruvuma na Sokoine (Lindi) ambapo kiasi cha sh. bilioni 2 zimetengwa huku shughuli ya kuwezesha mafunzo ya ubingwa bobezi nje ya nchi nazo zikitarajia kufanyika ambapo sh. bilioni tatu zimetengwa.

Vipaumbele vingine ni kugharamia mafunzo ya vitendo kwa wanafunzi tarajali (sh. bilioni 65), kuimarisha udhibiti wa magonjwa ya kuambukiza (sh. bilioni 12.6), kusimamia utekelezaji wa Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Ukimwi (sh. bilioni 26.6), kusimamia utekelezaji Mpango wa Kudhibiti Kifua Kikuu na Ukoma (sh. bilioni 14.8), huku kipaumbele cha 16 kikiwa kutekeleza afua mbalimbali za afya ambapo sh. bilioni 57.4 zimetengwa.

AJIRA MPYA

Ummy alisema pamoja na changamoto zinazoikabili sekta ya afya kutokana na upungufu wa rasilimali watu, wizara imeendelea kuchukua hatua mbalimbali kwa lengo la kupunguza pengo kati ya upatikanaji wa watumishi ikilinganishwa na mahitaji halisi.

“Katika kufikia azma hiyo, wizara imeendelea kuwasiliana na Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, tunamshukuru Rais Samia kwa kutoa kibali cha ajira mpya kwa wataalamu wa afya ambapo kwa mwaka 2022/2023 zimetengwa nafasi 10,285 za ajira,” alisisitiza.

MAOMBI YA FEDHA

Waziri Ummy aliliomba Bunge kuidhinisha sh. trilioni 1,109,421,722,000 ili kuweza kutekeleza malengo iliyojiwekea ambapo katika mwaka huo wa fedha, wizara imepanga kutumia kiasi cha sh. bilioni 554.2 kwa matumizi ya kawaida sawa na asilimia 50 ya bajeti tengwa, huku sh. bilioni 331.5 mishahara na sh. bilioni 222.7 kwa ajili ya matumizi mengineyo.

Kuhusu miradi ya maendeleo, alisema wizara yake inakadiria kutumia sh. bilioni 555.1 kwa ajili ya miradi ya maendeleo sawa na asilimia 50 ya bajeti tengwa. Kati ya hizo, fedha za ndani ni sh. bilioni 410.2 na fedha za nje ni sh. bilioni 144.8.

“Katika mwaka wa fedha 2022/2023, wizara na taasisi zilizo chini yake imekadiria kukusanya kiasi cha sh. bilioni 619.5, kati ya fedha hizo, sh. bilioni 140.8 zinatarajiwa kukusanywa kutoka vyanzo vya ndani makao makuu ya wizara, sh. bilioni 85.7 zitakusanywa katika hospitali za rufani za mikoa na sh. bilioni 392.9 zitakusanywa kutoka mashirika yaliyo chini ya wizara.

Alihitimisha kuwa: “Makusanyo hayo ni sawa na ongezeko la asilimia 22 ikilinganishwa na makadirio ya mwaka 2021/2022 ambayo yalikuwa sh. bilioni 507.2.”

KAMATI YASISITIZA MATUMIZI DAWA ASILI

Akiwasilisha maoni ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Stanslaus Nyongo, alisema kamati inaishauri serikali iwatambue watoa huduma za tiba asilia kwa kuwapa ithibati ili kuwahakikishia usalama wa afya zao wananchi wanapotumia huduma hizo.

Pia, alisema kamati hiyo inaishauri serikali kuweka utaratibu wa usambazaji wa tiba hizo asilia kama sehemu ya matibabu baada ya kupata ithibati ya matumizi yake.

“Ili kuepuka uwepo wa watoa huduma wasio waaminifu, kamati inashauri wizara iwasajili watoa huduma hao na dawa zao ambazo zimethibitika zinatibu magonjwa mbalimbali.

Aidha, serikali iendelee kutoa elimu kwa jamii kuhusu tiba asili na tiba mbadala ambazo hazina madhara kwa watumiaji,” alisisitiza.

NA MUSSA YUSUPH, DODOMA

Abdurahman Jumanne

Abdurahman Jumanne

Stay Connected test

  • 116 Follower
  • 172k Subscriber
  • 23.6k Follower
  • 99 Subscriber
  • Trending
  • Comments
  • Latest
MADAKTARI WAELEZEA JINSI YA KUZUIA MIMBA ISIHARIBIKE

MADAKTARI WAELEZEA JINSI YA KUZUIA MIMBA ISIHARIBIKE

July 9, 2021
TABWA YAMSIFU SAMIA KUWAPA FURSA WANAWAKE

TABWA YAMSIFU SAMIA KUWAPA FURSA WANAWAKE

July 9, 2021
BEI MPYA YA MBAAZI, KUNDE YAWAPANDISHA MZUKA WAKULIMA

BEI MPYA YA MBAAZI, KUNDE YAWAPANDISHA MZUKA WAKULIMA

August 9, 2021
MBUNGE LINDI ATAKA VIJANA WAJISHUGHULISHE

MBUNGE LINDI ATAKA VIJANA WAJISHUGHULISHE

July 8, 2021
NDUGU MATATANI KUMSHAMBULIA, KUMJERUHI MWENZAO KISA NG’OMBE

NDUGU MATATANI KUMSHAMBULIA, KUMJERUHI MWENZAO KISA NG’OMBE

0
WAHANDISI WA HALMASHAURI WAMEKUA WAKIIKOSEA SERIKALI KWAKUTOA TAARIFA ZA UONGO

WAHANDISI WA HALMASHAURI WAMEKUA WAKIIKOSEA SERIKALI KWAKUTOA TAARIFA ZA UONGO

0

OFISA ELIMU, MHANDISI, MKUU WA SHULE WAKALIA ‘KUTI KAVU’

0
STENDI YA ZAMANI UBUNGO  KUJENGWA DEPO MABASI MWENDOKASI

STENDI YA ZAMANI UBUNGO KUJENGWA DEPO MABASI MWENDOKASI

0
MIAKA 30 YA VYAMA VINGI: CHANGAMOTO NA MUSTAKABALI KUSONGA MBELE

MIAKA 30 YA VYAMA VINGI: CHANGAMOTO NA MUSTAKABALI KUSONGA MBELE

July 1, 2022
WAWILI WADAKWA DAR TUHUMA ZA BIASHARA YA NGONO MTANDAONI

WAWILI WADAKWA DAR TUHUMA ZA BIASHARA YA NGONO MTANDAONI

June 28, 2022
WAJUE WATIKISA NYAVU BORA 2021/2022

WAJUE WATIKISA NYAVU BORA 2021/2022

June 28, 2022
ATOZWA FAINI 100,000 KISA KUIBA PUNDA WA BABA YAKE

ATOZWA FAINI 100,000 KISA KUIBA PUNDA WA BABA YAKE

June 28, 2022

Recent News

MIAKA 30 YA VYAMA VINGI: CHANGAMOTO NA MUSTAKABALI KUSONGA MBELE

MIAKA 30 YA VYAMA VINGI: CHANGAMOTO NA MUSTAKABALI KUSONGA MBELE

July 1, 2022
WAWILI WADAKWA DAR TUHUMA ZA BIASHARA YA NGONO MTANDAONI

WAWILI WADAKWA DAR TUHUMA ZA BIASHARA YA NGONO MTANDAONI

June 28, 2022
WAJUE WATIKISA NYAVU BORA 2021/2022

WAJUE WATIKISA NYAVU BORA 2021/2022

June 28, 2022
ATOZWA FAINI 100,000 KISA KUIBA PUNDA WA BABA YAKE

ATOZWA FAINI 100,000 KISA KUIBA PUNDA WA BABA YAKE

June 28, 2022
Instagram Youtube Twitter Facebook

We are a diverse team of experts, innovative thinkers, creative designers, writers, innovators, strategists, pyschologists, comunictaors and web developers. UMG is extremely passionate about growing clients’ businesses, helping them achieve their goals and making a difference by raising the creative and communications industry standards in Tanzania.

Follow Us

Browse by Category

  • 2021
  • Afya Makala
  • BURUDANI
  • Business
  • GAZETI LA BURUDANI
  • GAZETI LA UHURU
  • GAZETI LA UHURU MACHI 17
  • HABARI KIMATAIFA
  • Habari Kitaifa
  • Habari Picha
  • KIMATAIFA
  • MAKALA
  • MAKALA AFYA
  • MAKALA-BURUDANI
  • MICHEZO
  • MICHEZO KIMATAIFA
  • MICHEZO KITAIFA
  • MICHEZO-MAKALA
  • MICHEZO-MASUMBWI
  • MITINDO
  • RIWAYA
  • SIASA
  • Uncategorized

Recent News

MIAKA 30 YA VYAMA VINGI: CHANGAMOTO NA MUSTAKABALI KUSONGA MBELE

MIAKA 30 YA VYAMA VINGI: CHANGAMOTO NA MUSTAKABALI KUSONGA MBELE

July 1, 2022
WAWILI WADAKWA DAR TUHUMA ZA BIASHARA YA NGONO MTANDAONI

WAWILI WADAKWA DAR TUHUMA ZA BIASHARA YA NGONO MTANDAONI

June 28, 2022

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

No Result
View All Result

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In