Monday, May 16, 2022
27 °c
Dar es Salaam
25 ° Thu
25 ° Fri
25 ° Sat
25 ° Sun
25 ° Mon
English EN Kiswahili SW
UHURU MEDIA GROUP
Tangaza Nasi
  • Mwanzo
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHAKA ANG’AKA FAINI MIMBA ZA WANAFUNZI

    NI HISTORIA NYINGINE CCM

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM YATEUA MAKATIBU WA MIKOA NA WILAYA

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM ITAENDELEA KUWA CHAMA BORA, IMARA AFRIKA- SHAKA

    MBISE ATOA VITI MIA MOJA MONDULI

    MBISE ATOA VITI MIA MOJA MONDULI

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
  • Michezo
    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    PABLO AIPANIA KMC 

    PABLO AIPANIA KMC 

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
  • UMG
    • Home
    • About Us
    • Services
    • Shop
    • Contact Us
  • MAGAZETI
    • Uhuru wanawake
    • Mzalendo
    • Uhuru vijijini
    • Burudani
    • Uhuru kijani
  • UHURU FM
    • Ratiba
  • UHURU DIGITAL
    • Instagram
    • Facebook
    • Twitter
    • Youtube
  • Mwanzo
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHAKA ANG’AKA FAINI MIMBA ZA WANAFUNZI

    NI HISTORIA NYINGINE CCM

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM YATEUA MAKATIBU WA MIKOA NA WILAYA

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM ITAENDELEA KUWA CHAMA BORA, IMARA AFRIKA- SHAKA

    MBISE ATOA VITI MIA MOJA MONDULI

    MBISE ATOA VITI MIA MOJA MONDULI

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
  • Michezo
    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    PABLO AIPANIA KMC 

    PABLO AIPANIA KMC 

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
No Result
View All Result
UHURU MEDIA GROUP
No Result
View All Result
Mwanzo Habari Kitaifa

MBOWE, WENZAKE WAGONGA MWAMBA MAHAKAMA KUU

>>Ni baada ya mapingamizi yao kutupiliwa mbali

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
October 20, 2021
in Habari Kitaifa
0 0
0
MBOWE, WENZAKE WAGONGA MWAMBA MAHAKAMA KUU
0
SHARES
104
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

MAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, imetupilia mbali mapingamizi yaliyowasilishwa na mawakili wa utetezi katika kesi inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe na kuamua kupokea maelezo ya onyo ya mshitakiwa Adam Kasekwa kama kielelezo cha upande wa Jamhuri.

Aidha, Jaji Kiongozi Mustapher Siyani, ametangaza kujitoa kusikiliza shauri hilo kwasababu ya majukumu mpya aliyonayo huku akieleza kuwa uhasilia wa kesi hiyo inatakiwa kusikilizwa mfululizo, ili kujulikana hatima yake.

Hayo yalijiri mahakamani hapo, wakati shauri hilo lilipopelekwa kwa kutolewa uamuzi wa kesi ndogo ndani ya kesi wa ama kupokelewa au la maelezo ya onyo yanayodaiwa kutolewa na mshitakiwa Kasekwa.

Kesi ndogo ndani ya kesi ya msingi ilitokana na upande wa utetezi ukiongozwa na Wakili Peter Kibatala, kupinga kupokelewa kwa maelezo hayo kwa madai kabla na baada ya kuchukuliwa mshitakiwa aliteswa na yalichukuliwa nje ya muda kwa mujibu wa sheria.

Mbali na Mbowe na Kasekwa, washitakiwa wengine katika kesi ya msingi ni Mohamed Ling’wenya na Moses Lijenje, wanaokabiliwa na mashitaka ya

Ugaidi.

Akisoma uamuzi huo, Jaji Kiongozi Siyani alisema anapokea maelezo hayo kwasababu ushahidi wa upande wa utetezi uliotolewa mahakamani hapo hauendani na pingamizi lililowasilishwa.

Kuhusu hoja ya kwamba maelezo yalichukuliwa nje ya muda, Jaji Kiongozi Siyani alisema maelezo yalichukuliwa ndani ya muda ambao askari  waliutumia kumtafuta mtukumiwa Lijenje aliyekuwa na Kasekwa.

Pia, alisema hakuna ubishi kwamba washitakiwa hawakukataa walikuwa na Lijenje katika eneo la tukio, Rau Madukani Moshi, ambapo askari  walifanikiwa kuwakamata washitakiwa (Kasekwa na Mohamed Ling’wenya), badala ya watatu jambo lililowalazimu kushirikiana na polisi kumtafuta Lijenje.

Alisema katika kesi hiyo, polisi walikuwa na sababu ya kuchelewa kuchukuwa maelezo ya mshitakiwa kwa kuwa shughuli za kiupelelezi zilizokuwa zikiendelea na kumtafuta  Lijenje na kuwasafirisha watuhumiwa kutoka Moshi hadi Dar es Salaam.

Katika hoja ya kwamba maelezo yalichukuliwa mshitakiwa  akiwa katika mateso,  Jaji Siyani alisema mshitakiwa alikubali kutoa maelezo, lakini hakuna ushahidi wa kwamba hakufika Kituo cha Polisi cha Kati Dar es Salaam, yalipochukuliwa maelezo hayo.

Alisema katika ushahidi wa upande wa utetezi, hakuna mahali upande huo ulibainisha Kasekwa hakufika kituo hicho cha polisi.

Jaji huyo alieleza kuwa wakati shahidi wa kwanza wa upande wa Jamhuri, Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Kinondoni, Ramadhan Kingai akitoa ushahidi wake aliieleza Mahakama kwamba maelezo ya onyo ya Kasekwa yalichukuliwa kituoni hapo kuanzia saa moja na nusu hadi saa tatu asubuhi, lakini hakuna panapobishaniwa kuwa hakufika kituoni hapo.

Alisema maelezo ya shahidi yanakinzana na hoja ya msingi ya kuteswa kwake na kwamba hakuna ubishi kuwa Kasekwa alitoa maelezo kwa ridhaa yake na kwa hali hiyo, hivyo ameyapokea maelezo hayo kama kielelezo namba moja cha upande wa Jamhuri.

Kasekwa katika ushahidi wake mahakamani hapo, alikana kuongoza askari kumtafuta Lijenje,  kupelekwa Kituo cha Polisi cha Kati  Agosti 7, mwaka 2020 na alipelekwa kituo cha Polisi Tazara kisha Mbweni na waliomkamata walimtesa na alilazimishwa kutoa maelezo na kutia saini nyaraka akiwa Mbweni Agosti 9, mwaka 2020.

JAJI AJITOA

Akitangaza uamuzi wa kujitoa kusikiliza kesi hiyo, Jaji Siyani alisema amefikia uamuzi huo kwasababu ya majukumu mpya aliyonayo huku akieleza kuwa kwa uhasilia wa kesi hiyo inatakiwa kusikilizwa mfululizo, ili kujulikana hatima yake.

“Kutokana na majukumu haya sitaweza kusikiliza, hivyo naona  ni busara kujitoa ili msajili wa Mahakama ampangie Jaji mwingine ambaye ataendelea pale alipoishia.”

“Nawashukuru wote mliokuwa mkihudhuria kesi hii kwa kipindi chote kwa kusikiliza. Hivyo najitoa rasmi na msajili atapanga jaji atakayesikiliza, jina la Jaji atakayekuja na tarehe msajili atasema,” alisema.

Jaji Kiongozi Siyani alisema kesi hiyo itakapopelekwa tena mahakamani hapo inatarajiwa kuendelea kwa ushahidi wa shahidi wa kwanza wa upande wa Jamhuri Kingai aendelee kutoa ushahidi wake pale alipoishia.

Hivi karibuni Jaji Siyani aliteuliwa na Rais Samia Suluhu Hassan kuwa Jaji Kiongozi akichukuwa nafasi ya aliyekuwa Jaji Kiongozi, Eliezar Fereshi, aliyeteuliwa kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG).

Huyo ni Jaji wa pili kujitoa kusikiliza kesi hiyo, ambapo Jaji wa kwanza alikuwa Elinaza Luvanda ambaye alijitoa baada ya washitakiwa kumuomba afanye hivyo kwa kuwa hawakuwa na imani naye.

Askofu afanya maombi mahakamani

Kabla Jaji Siyani hajaingia mahakamani na kesi kuanza kusikilizwa, Askofu Mkuu wa Kanisa la Moravian Uamsho, Emmaus Mwamakula alifanya maombi kwa kuwaombea washitakiwa hao pamoja na mawakili wa utetezi.

Askofu huyo alifanya maombi kwa kuanza kuombea jopo la Mawakili wa utetezi na baadaye Mbowe na washitakiwa wenzake walipoingizwa ndani ya chumba cha mahakama pia aliwaombea.

Maombi hayo yalifanyika kwa mawakili hao kusimama kwa pamoja na askofu huyo huku wakionekana kuinamisha vichwa kwa dakika kadhaa.

Katika kesi hiyo, washitakiwa wanakabiliwa na mashitaka sita ya kula njama kutenda makosa ya ugaidi, kukutwa na mali iliyokusuduwa kutumika kutenda vitendo vya kigaidi na kufadhili vitendo vya kigaidi linalomkabili Mbowe.

NA REHEMA MOHAMED 

Abdurahman Jumanne

Abdurahman Jumanne

Stay Connected test

  • 110 Follower
  • 168k Subscriber
  • 23.5k Follower
  • 99 Subscriber
  • Trending
  • Comments
  • Latest
MADAKTARI WAELEZEA JINSI YA KUZUIA MIMBA ISIHARIBIKE

MADAKTARI WAELEZEA JINSI YA KUZUIA MIMBA ISIHARIBIKE

July 9, 2021
TABWA YAMSIFU SAMIA KUWAPA FURSA WANAWAKE

TABWA YAMSIFU SAMIA KUWAPA FURSA WANAWAKE

July 9, 2021
BEI MPYA YA MBAAZI, KUNDE YAWAPANDISHA MZUKA WAKULIMA

BEI MPYA YA MBAAZI, KUNDE YAWAPANDISHA MZUKA WAKULIMA

August 9, 2021
MBUNGE LINDI ATAKA VIJANA WAJISHUGHULISHE

MBUNGE LINDI ATAKA VIJANA WAJISHUGHULISHE

July 8, 2021
MAJALIWA ATOA MAAGIZO KWA TAASISI ZA MAPATO

MAJALIWA ATOA MAAGIZO KWA TAASISI ZA MAPATO

0
SERIKALI YAITA WASHIRIKA UTEKELEZAJI SENSA 2022

SERIKALI YAITA WASHIRIKA UTEKELEZAJI SENSA 2022

0
SMZ YAWASISITIZA WANANCHI KUPATA CHANJO YA UVIKO-19

WAJASIRIAMALI Z’BAR WAPEWA MCHONGO FEDHA ZA UVIKO-19

0
TTCL YAJIVUNIA UTOAJI HUDUMA WA MAWASILIANO KIMATAIFA

TTCL YAJIVUNIA UTOAJI HUDUMA WA MAWASILIANO KIMATAIFA

0
SHAKA:UAMUZI KUWAPANGA WAMACHINGA USIPOTOSHWE

SHAKA:UAMUZI KUWAPANGA WAMACHINGA USIPOTOSHWE

May 16, 2022
WAZIRI AAGIZA BABA ANAYEDAIWA KUBAKA MWANAWE AKAMATWE

WAZIRI AAGIZA BABA ANAYEDAIWA KUBAKA MWANAWE AKAMATWE

May 16, 2022
CCM YAGUSWA NYONGEZA YA MISHAHARA KWA WATUMISHI

CCM YAGUSWA NYONGEZA YA MISHAHARA KWA WATUMISHI

May 16, 2022
UWT TEMEKE KUMUUNGA MKONO RAIS SAMIA

UWT TEMEKE KUMUUNGA MKONO RAIS SAMIA

May 11, 2022

Recent News

SHAKA:UAMUZI KUWAPANGA WAMACHINGA USIPOTOSHWE

SHAKA:UAMUZI KUWAPANGA WAMACHINGA USIPOTOSHWE

May 16, 2022
WAZIRI AAGIZA BABA ANAYEDAIWA KUBAKA MWANAWE AKAMATWE

WAZIRI AAGIZA BABA ANAYEDAIWA KUBAKA MWANAWE AKAMATWE

May 16, 2022
CCM YAGUSWA NYONGEZA YA MISHAHARA KWA WATUMISHI

CCM YAGUSWA NYONGEZA YA MISHAHARA KWA WATUMISHI

May 16, 2022
UWT TEMEKE KUMUUNGA MKONO RAIS SAMIA

UWT TEMEKE KUMUUNGA MKONO RAIS SAMIA

May 11, 2022
Instagram Youtube Twitter VK Facebook

We are a diverse team of experts, innovative thinkers, creative designers, writers, innovators, strategists, pyschologists, comunictaors and web developers. UMG is extremely passionate about growing clients’ businesses, helping them achieve their goals and making a difference by raising the creative and communications industry standards in Tanzania.

Follow Us

Browse by Category

  • 2021
  • Afya Makala
  • BURUDANI
  • Business
  • GAZETI LA BURUDANI
  • GAZETI LA UHURU
  • GAZETI LA UHURU MACHI 17
  • HABARI KIMATAIFA
  • Habari Kitaifa
  • Habari Picha
  • KIMATAIFA
  • MAKALA
  • MAKALA AFYA
  • MAKALA-BURUDANI
  • MICHEZO
  • MICHEZO KIMATAIFA
  • MICHEZO KITAIFA
  • MICHEZO-MAKALA
  • MICHEZO-MASUMBWI
  • MITINDO
  • RIWAYA
  • SIASA
  • Uncategorized

Recent News

SHAKA:UAMUZI KUWAPANGA WAMACHINGA USIPOTOSHWE

SHAKA:UAMUZI KUWAPANGA WAMACHINGA USIPOTOSHWE

May 16, 2022
WAZIRI AAGIZA BABA ANAYEDAIWA KUBAKA MWANAWE AKAMATWE

WAZIRI AAGIZA BABA ANAYEDAIWA KUBAKA MWANAWE AKAMATWE

May 16, 2022

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

No Result
View All Result

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In