Monday, May 16, 2022
27 °c
Dar es Salaam
25 ° Thu
25 ° Fri
25 ° Sat
25 ° Sun
25 ° Mon
English EN Kiswahili SW
UHURU MEDIA GROUP
Tangaza Nasi
  • Mwanzo
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHAKA ANG’AKA FAINI MIMBA ZA WANAFUNZI

    NI HISTORIA NYINGINE CCM

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM YATEUA MAKATIBU WA MIKOA NA WILAYA

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM ITAENDELEA KUWA CHAMA BORA, IMARA AFRIKA- SHAKA

    MBISE ATOA VITI MIA MOJA MONDULI

    MBISE ATOA VITI MIA MOJA MONDULI

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
  • Michezo
    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    PABLO AIPANIA KMC 

    PABLO AIPANIA KMC 

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
  • UMG
    • Home
    • About Us
    • Services
    • Shop
    • Contact Us
  • MAGAZETI
    • Uhuru wanawake
    • Mzalendo
    • Uhuru vijijini
    • Burudani
    • Uhuru kijani
  • UHURU FM
    • Ratiba
  • UHURU DIGITAL
    • Instagram
    • Facebook
    • Twitter
    • Youtube
  • Mwanzo
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHAKA ANG’AKA FAINI MIMBA ZA WANAFUNZI

    NI HISTORIA NYINGINE CCM

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM YATEUA MAKATIBU WA MIKOA NA WILAYA

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM ITAENDELEA KUWA CHAMA BORA, IMARA AFRIKA- SHAKA

    MBISE ATOA VITI MIA MOJA MONDULI

    MBISE ATOA VITI MIA MOJA MONDULI

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
  • Michezo
    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    PABLO AIPANIA KMC 

    PABLO AIPANIA KMC 

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
No Result
View All Result
UHURU MEDIA GROUP
No Result
View All Result
Mwanzo Habari Kitaifa

MIAKA 60 YA UHURU WANAOMILIKI ARDHI WAFIKIA MILIONI 2 KUTOKA 26,499

MAFANIKIO>>Maduhuli yatokanayo na ardhi yameongezeka kutoka sh. bilioni 1.4 hadi sh. bilioni 121

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 22, 2021
in Habari Kitaifa
0 0
0
MIAKA 60 YA UHURU WANAOMILIKI ARDHI WAFIKIA MILIONI 2 KUTOKA 26,499

WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi

0
SHARES
56
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

SERIKALI imesema katika kipindi cha miaka 60 ya Uhuru, inajivunia kuona idadi ya Watanzania wanaomiliki ardhi imeongezeka kutoka 26,499 kabla ya Uhuru hadi kufikia 2,067,044.

Imesema kwa kutambua umuhimu wa kuboresha makazi ya wananchi ilianzisha kampuni ya kutoa mikopo ya gharama nafuu kwa benki ili wananchi wakope fedha za ujenzi wa nyumba.

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi, aliyasema hayo jijini Dodoma, alipokuwa akitoa mafanikio ya miaka 60 ya Uhuru ya wizara hiyo.

Lukuvi alisema tangu Uhuru hadi sasa serikali inajivunia kuona wananchi wake wanaishi katika makazi bora zaidi ikilinganishwa na  kabla ya Uhuru.

“Katika kipindi cha miaka 60 ya Uhuru tuna miliki za ardhi 2,067,044, vyeti vya ardhi ya kijiji 11,744 na hati za hakimiliki za kimila 867,148 zimetolewa,” alisema.

Waziri Lukuvi aliongeza kuwa: “Leseni za makazi 112,787 zimetolewa kwa wananchi waishio maeneo yasiyopangwa mijini na baadhi ya wananchi wanazitumia hati hizo kama dhamana kupata mikopo katika taasisi za fedha kwa shughuli za kiuchumi.”

KUBORESHA MAKAZI

Lukuvi alisema baada ya kupata Uhuru mwaka 1961, serikali ilianza kuboresha mazingira ya uendelezaji milki nchini na kuanzisha Shirika la Nyumba la Taifa (NHC).

Aliongeza kuwa mwaka 1992, serikali ilianzisha Mfuko wa Mikopo ya Nyumba kwa Watumishi wa Serikali ili kuwasaidia kupata mikopo yenye masharti nafuu ya kujenga nyumba za kuishi.

Waziri alisema hadi sasa serikali imetoa mikopo ya nyumba yenye thamani ya sh. 9,159,902,229.85 kwa watumishi takriban 1,689.

“Serikali kwa kutambua umuhimu wa kuboresha makazi ya wananchi ilianzisha kampuni ya kutoa mikopo ya gharama nafuu kwa benki ili kuwezesha wananchi kukopa fedha kwa ajili ya ujenzi wa nyumba. Hadi sasa taasisi za kifedha 32 zinatoa mikopo kwa wananchi,” alisema Lukuvi.

Lukuvi alisema serikali imeshatoa sh. bilioni 474.5 za kuwawezesha wananchi katika ujenzi wa nyumba, lengo ni kuboresha ustawi wa jamii katika maeneo ya vijijini.

UPIMAJI ARDHI

Kuhusu upimaji ardhi, Waziri Lukuvi alisema mafanikio makubwa zaidi yaliyopatikana katika masuala ya upimaji ni upatikanaji wa vifaa vya kisasa na usimikaji wa miundombinu ya kisasa ya upimaji yenye kurahisisha upimaji.

Alisema kwa sasa kuna kasi kubwa ya upimaji wa ardhi na utoaji wa hati miliki kwa kuwa wamezingatia vifaa vya kisasa vya kuandalia ramani za msingi kwa ajili ya kuwezesha utayarishaji na uchapaji ramani.

Alibainisha kuwa serikali imenunua ndege isiyokuwa na rubani maalumu ya upigaji picha za anga zinazowezesha uandaaji wa ramani za msingi na kuzifanyia marejeo.

“Kutokana na mfumo na vifaa vya kisasa, viwanja 2,783,278 na mashamba 28,784 yamepimwa nchini kote na kwa sasa kasi imeongezeka zaidi, tumepeleka sh. bilioni 50 katika halmashauri nchini kwa ajili ya kupanga, kupima na kumilikisha ardhi,” alisema Lukuvi.

SAKATA LA MADALALI

Waziri Lukuvi alisema Desemba 13, mwaka huu, anatarajia kukutana na madalali wa nyumba na viwanjaa jijini Dar es Salaam ili kupanga mikakati ya namna watakavyotekeleza majukumu yao.

Alisema hali hiyo inatokana na mwenendo wa ufanyaji kazi umekuwa si wa kuridhisha na kuzua taharuki kwa jamii.

“Nitakutana nao ili tuangalie mustakabali wa suala lao, naamini hapa hakuna kinachoshindikana kila kitu kitakuwa sawa tunataka kila mtu afanye kazi yake kwa usahihi,” alisema Lukuvi.

UTATUZI WA MIGOGORO

Lukuvi alisema baada ya Uhuru, utatuzi wa migogoro ya ardhi ulikuwa unafanyika kupitia mabaraza ya kimila na mfumo wa mahakama za kawaida.

Hata hivyo, utatuzi wa migogoro ya ardhi kupitia mfumo wa mahakama ulibainika kuwa na changamoto za mlundikano wa mashauri na matumizi ya mbinu nyingi za kisheria.

“Kutokana na kukithiri kwa migogoro ya matumizi ya ardhi baina ya makundi  mbalimbali nchini serikali iliunda kamati ya mawaziri ya kisekta ya wizara nane mwaka 2018, inayojumuisha Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

“Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI); Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira); Maliasili na Utalii; Mifugo na Uvuvi; Kilimo; Maji; na Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa ili kutafuta ufumbuzi wa kudumu wa migogoro hiyo,” alisema.

Aliongeza kuwa: “Baadhi ya mapendekezo yaliyotolewa na kamati hiyo na kuridhiwa na Baraza la Mawaziri, Septemba, 2019 ni kuhalalishwa rasmi kwa vijiji 920 kati ya vijiji 975 vilivyokuwemo ndani ya hifadhi, mapori ya akiba na ranchi kwa ajili ya shughuli za kilimo, ufugaji na kijamii.”

Waziri lukuvi alisema ili kupunguza migogoro ya ardhi wameanzisha mfumo wa kielektroniki, ambapo mtu akiomba kiwanja itaonyesha katika mfumo kama kinamilikiwa na mtu au la.

Hatua hiyo imekuja baada ya kubaini chanzo cha migogoro mingi na kutolea mfano Dodoma, inasababishwa na utoaji umiliki sehemu moja kwa watu tofauti zaidi ya mmoja.

PATO LA TAIFA

Kwa mujibu wa waziri huyo, umilikishaji wa ardhi kwa wananchi umewapa fursa wananchi kuchangia pato la Taifa.

Alisema serikali inakusanya maduhuli ya sekta ya ardhi kutoka katika vyanzo mbalimbali kama vile kodi ya Pango la Ardhi, Ada za Upimaji wa Ardhi na Machapisho mbalimbali Ada ya Uthamini,  Ada za Usajili wa Hati na Nyaraka Mbalimbali.

Waziri alisema kwa miaka 10 ya hivi karibuni Juni, 2011 hadi Jalai, 2021 wamekusanya sh. bilioni 735.8, hivyo maduhuli yatokanayo na sekta ya ardhi yameongezeka kutoka sh.bilioni 1.4 kwa mwaka wa fedha 1996/97 hadi kufikia sh. bilioni 121 katika mwaka wa fedha 2020/21.

“Na kwa mwaka huu (2021/2022) tuna malengo ya kukusanya bilioni 221. Matarajio ni kuhakikisha sekta hii inachangia zaidi katika pato la Taifa ikiwemo mapato ya kodi,” alisema.

NA FRED ALFRED DODOMA

Abdurahman Jumanne

Abdurahman Jumanne

Stay Connected test

  • 110 Follower
  • 168k Subscriber
  • 23.5k Follower
  • 99 Subscriber
  • Trending
  • Comments
  • Latest
MADAKTARI WAELEZEA JINSI YA KUZUIA MIMBA ISIHARIBIKE

MADAKTARI WAELEZEA JINSI YA KUZUIA MIMBA ISIHARIBIKE

July 9, 2021
TABWA YAMSIFU SAMIA KUWAPA FURSA WANAWAKE

TABWA YAMSIFU SAMIA KUWAPA FURSA WANAWAKE

July 9, 2021
BEI MPYA YA MBAAZI, KUNDE YAWAPANDISHA MZUKA WAKULIMA

BEI MPYA YA MBAAZI, KUNDE YAWAPANDISHA MZUKA WAKULIMA

August 9, 2021
MBUNGE LINDI ATAKA VIJANA WAJISHUGHULISHE

MBUNGE LINDI ATAKA VIJANA WAJISHUGHULISHE

July 8, 2021
SHAKA AWAHIMIZA WATANZANIA KUCHAPAKAZI KUINUA UCHUMI

SHAKA AWAHIMIZA WATANZANIA KUCHAPAKAZI KUINUA UCHUMI

0
TTCL YAJIVUNIA UTOAJI HUDUMA WA MAWASILIANO KIMATAIFA

TTCL YAJIVUNIA UTOAJI HUDUMA WA MAWASILIANO KIMATAIFA

0
KIKONGWE KUHITIMU PHD

KIKONGWE KUHITIMU PHD

0
MKUTANO WA KIHISTORIA KATIKA HISTORIA YA MIAKA 100 YA CPC

MKUTANO WA KIHISTORIA KATIKA HISTORIA YA MIAKA 100 YA CPC

0
UWT TEMEKE KUMUUNGA MKONO RAIS SAMIA

UWT TEMEKE KUMUUNGA MKONO RAIS SAMIA

May 11, 2022
DK. MWINYI ASEMA HAKI KICHOCHEO CHA AMANI NCHNI

DK. MWINYI ASEMA HAKI KICHOCHEO CHA AMANI NCHNI

May 11, 2022
SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

May 11, 2022
MABEHEWA MAPYA 22 KUNUNULIWA

MABEHEWA MAPYA 22 KUNUNULIWA

May 11, 2022

Recent News

UWT TEMEKE KUMUUNGA MKONO RAIS SAMIA

UWT TEMEKE KUMUUNGA MKONO RAIS SAMIA

May 11, 2022
DK. MWINYI ASEMA HAKI KICHOCHEO CHA AMANI NCHNI

DK. MWINYI ASEMA HAKI KICHOCHEO CHA AMANI NCHNI

May 11, 2022
SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

May 11, 2022
MABEHEWA MAPYA 22 KUNUNULIWA

MABEHEWA MAPYA 22 KUNUNULIWA

May 11, 2022
Instagram Youtube Twitter VK Facebook

We are a diverse team of experts, innovative thinkers, creative designers, writers, innovators, strategists, pyschologists, comunictaors and web developers. UMG is extremely passionate about growing clients’ businesses, helping them achieve their goals and making a difference by raising the creative and communications industry standards in Tanzania.

Follow Us

Browse by Category

  • 2021
  • Afya Makala
  • BURUDANI
  • Business
  • GAZETI LA BURUDANI
  • GAZETI LA UHURU
  • GAZETI LA UHURU MACHI 17
  • HABARI KIMATAIFA
  • Habari Kitaifa
  • Habari Picha
  • KIMATAIFA
  • MAKALA
  • MAKALA AFYA
  • MAKALA-BURUDANI
  • MICHEZO
  • MICHEZO KIMATAIFA
  • MICHEZO KITAIFA
  • MICHEZO-MAKALA
  • MICHEZO-MASUMBWI
  • MITINDO
  • RIWAYA
  • SIASA
  • Uncategorized

Recent News

UWT TEMEKE KUMUUNGA MKONO RAIS SAMIA

UWT TEMEKE KUMUUNGA MKONO RAIS SAMIA

May 11, 2022
DK. MWINYI ASEMA HAKI KICHOCHEO CHA AMANI NCHNI

DK. MWINYI ASEMA HAKI KICHOCHEO CHA AMANI NCHNI

May 11, 2022

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

No Result
View All Result

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In