Sunday, July 3, 2022
27 °c
Dar es Salaam
25 ° Thu
25 ° Fri
25 ° Sat
25 ° Sun
25 ° Mon
English EN Kiswahili SW
UHURU MEDIA GROUP
Tangaza Nasi
  • Mwanzo
  • Siasa
    • All
    • Business
    MEMBE ATOA YA MOYONI AKIREJEA CCM

    MEMBE ATOA YA MOYONI AKIREJEA CCM

    SHAKA ANG’AKA FAINI MIMBA ZA WANAFUNZI

    NI HISTORIA NYINGINE CCM

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM YATEUA MAKATIBU WA MIKOA NA WILAYA

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM ITAENDELEA KUWA CHAMA BORA, IMARA AFRIKA- SHAKA

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
  • Michezo
    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    PABLO AIPANIA KMC 

    PABLO AIPANIA KMC 

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
  • UMG
    • Home
    • About Us
    • Services
    • Shop
    • Contact Us
  • MAGAZETI
    • Uhuru wanawake
    • Mzalendo
    • Uhuru vijijini
    • Burudani
    • Uhuru kijani
  • UHURU FM
    • Ratiba
  • UHURU DIGITAL
    • Instagram
    • Facebook
    • Twitter
    • Youtube
  • Mwanzo
  • Siasa
    • All
    • Business
    MEMBE ATOA YA MOYONI AKIREJEA CCM

    MEMBE ATOA YA MOYONI AKIREJEA CCM

    SHAKA ANG’AKA FAINI MIMBA ZA WANAFUNZI

    NI HISTORIA NYINGINE CCM

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM YATEUA MAKATIBU WA MIKOA NA WILAYA

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM ITAENDELEA KUWA CHAMA BORA, IMARA AFRIKA- SHAKA

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
  • Michezo
    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    PABLO AIPANIA KMC 

    PABLO AIPANIA KMC 

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
No Result
View All Result
UHURU MEDIA GROUP
No Result
View All Result
Mwanzo Habari Kitaifa

MIPAKA YA TANZANIA IPO SHWARI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
May 20, 2022
in Habari Kitaifa
0 0
0
MIPAKA YA TANZANIA IPO SHWARI

WAZIRI wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Stergomena Tax.

0
SHARES
37
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

WAZIRI wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Stergomena Tax, amesema hali ya ulinzi na usalama katika mipaka ya Tanzania yenye urefu wa kilometa 5,461.20 na kuhusisha eneo la nchi kavu na majini, ipo shwari

Mipaka hiyo ni baina ya Tanzania na Msumbiji, Malawi, Zambia, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Burundi, Rwanda, Uganda na Kenya.

Akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi kwa wizara hiyo katika mwaka wa Fedha 2022/2023, Waziri huyo amesema katika kipindi hicho hapakuwa na matukio ya uhasama yaliyoripotiwa baina Tanzania na nchi zinazopakana, licha ya kuwepo changamoto kadhaa.

MPAKA WA TANZANIA NA DRC

Stergomena alisema hali ya usalama wa mpaka huo ni shwari kwani hakuna tukio la kuhatarisha usalama kwa nchi.

Hata hivyo, alisema ndani ya DRC yameripotiwa matukio ya waasi kushambulia miji mbalimbali nchini humo.

“Wizara kupitia Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) imeendelea kuwa macho na kujipanga wakati wote. Aidha, ushiriki wa Tanzania katika misheni ya Umoja wa Mataifa (UN) katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (United Nations Organisation Stabilization Mission in the Democratic Republic of the Congo – MONUSCO) unaisaidia nchi kujiimarisha kiulinzi ipasavyo,” alisisitiza.

MPAKA TANZANIA NA MALAWI

Stergomena alieleza kuwa hali ya usalama ya mpaka huo ni shwari na hakuna tukio la kuhatarisha usalama lililoripotiwa.

Alisisitiza kuwa ushirikiano uliopo baina ya Jeshi la Tanzania na Jeshi la Malawi ni mzuri na inajidhihirisha kutokana na mahusiano mazuri yaliyopo ambayo yamesababisha kufanyika michezo ya kirafiki kati ya timu za majeshi ya nchi hizi mbili yaliyofanyika Brigedi ya Kusini, Julai mwaka jana.

“Changamoto ya mpaka katika Ziwa Nyasa inaendelea kufanyiwa kazi kupitia Tume Maalum ya Usuluhishi (High Level Mediation Team) iliyoundwa na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).

“Serikali yetu kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inaendelea kutumia njia za kidiplomasia ili kulipatia ufumbuzi wa kudumu suala hilo,” alieleza.

Kuhusu hali ya mpaka wa Tanzania na Zambia, alisema hali ya usalama katika mpaka huo ni shwari na hakuna tukio la kuhatarisha usalama wa nchi lililoripotiwa hadi sasa.

MPAKA TANZANIA NA BURUNDI

Akieleza hali ya usalama wa mpaka huo, alisema hali ni shwari kwani hakuna matukio yoyote yaliyoripotiwa kuhatarisha usalama baina ya nchi hizo, ingawa eneo hilo linakabiliwa na uwepo wa wahamiaji haramu, uvamizi wa wakulima na uingizaji wa mifugo kwa ajili ya kupata malisho ambapo JWTZ imeendelea kukabiliana na hali hiyo.

MPAKA TANZANIA NA RWANDA

Waziri huyo wa ulinzi alisema usalama wa mpaka huo ni shwari, ingawa yapo matukio machache ya kihalifu ya wahamiaji haramu na uingizaji wa mifugo kwa ajili ya malisho. Wizara kupitia JWTZ inaendelea kuchukua hatua za kudhibiti matukio hayo.

MPAKA TANZANIA NA UGANDA

Stergomena alibainisha kuwa hali ya usalama katika mpaka huo ni shwari na hakuna tukio la kuhatarisha usalama wa nchi.

Hata hivyo, alieleza uwepo wa changamoto ya uingizaji haramu wa mifugo kwa ajili ya malisho.

Alisema juhudi za kuimarisha mpaka zinaendelea kwa kuongeza alama kati ya marundo ya mawe yaliyowekwa na mkoloni, na kujenga barabara ya usalama kwenye Mpaka

MPAKA TANZANIA NA KENYA

Alieleza kuwa hali ya usalama wa mpaka baina ya Tanzania na Kenya ni shwari na hakuna tukio la kuhatarisha usalama dhidi ya Tanzania lililoripotiwa.

Alibainisha kuwa ipo changamoto ya kuharibiwa kwa alama za mpaka na kazi ya kuimarisha mpaka huo inayotekelezwa na timu ya wataalam kutoka Tanzania na Kenya inaendelea vizuri, ambapo awamu ya kwanza imeanzia eneo la Serengeti hadi Ziwa Natron.

MPAKA WA TANZANIA BAHARI YA HINDI

Kuhusu mpaka wa Tanzania katika Bahari ya Hindi, alisema hali yake ni shwari.

Waziri huyo alieleza kuwa katika mpaka huo Tanzania imepakana na nchi za Comoro na Shelisheli.

“Hakuna tukio lililoripotiwa la kuhatarisha usalama dhidi ya Tanzania. Aidha, JWTZ imeendelea kufanya doria za mara kwa mara katika eneo la Bahari ya Hindi ili kubaini na kuzuia wahamiaji haramu, usafirishaji haramu wa binadamu, usafirishaji wa dawa za kulevya na matishio ya kigaidi,” alibainisha.

MPAKA WA TANZANIA NA MSUMBIJI

Kwa mujibu wa waziri huyo wa ulinzi, alisema hali ya usalama wa mpaka huo ni ya wastani kutokana na mashambulizi yanayofanywa na kundi la kigaidi la Ansar Al Sunna Wal Jamaah (AASWJ) maeneo ya Kaskazini mwa Msumbiji, katika Jimbo la Cabo Delgado linalopakana na Mkoa wa Mtwara.

Alisema kundi hilo limekuwa likiathiri usalama kwa kuharibu na kupora mali za wananchi.

“Katikakupambananachangamoto hii, JWTZ imeendelea kuimarisha ulinzi kwa kufanya operesheni za ndani ya nchi kukabiliana na kundi hilo. Aidha, JWTZ inashiriki operesheni chini ya Mwamvuli wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika nchini Msumbiji (SADC Mission in Mozambique – SAMIM) katika jitihada za kudhibiti ugaidi.

Aliongeza kuwa: “Operesheni hizi zimeendelea kuimarisha ulinzi katika eneo la Mpaka, kudumisha amani na utulivu.”

Stergomena alisema operesheni hizo zimesaidia kupunguza nguvu ya kundi hilo la kigaidi, hata hivyo, kundi hilo linatekeleza mashambulizi kwa kuhamahama na kubadili mbinu za kimapigano.

Licha ya hali hiyo, alisema Tanzania inaendelea kupambana kuhakikisha kundi hilo halileti madhara zaidi.

“Wizara inaishukuru Serikali hususani, Rais na Amiri Jeshi Mkuu, Samia Suluhu Hassan, kwa kutoa kipaumbele katika kupambana na suala hili, kutoa fedha kwa ajili ya mahitaji mbalimbali yanayosaidia vikundi vya ulinzi kupambana dhidi ya kundi hilo,” alieleza.

Stergomena alisema katika mwaka wa fedha 2022/2023, Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, imelenga kutekeleza mpango na bajeti kwa kuzingatia mambo Dira na Dhima ya Wizara, Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025 na Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano (2021/22 – 2025/26).

Aliyataja mambo mengine yatakayozingatiwa katika bejeti hiyo ni Malengo ya Maendeleo Endelevu 2030 (SDGs), Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya Mwaka 2020 na Mwongozo wa Maandalizi ya Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023.

Alibainisha kuwa katika mwaka huo wa fedha, serikali inatarajia kutenga fedha kwa ajili ya matumizi ya kawaida na maendeleo, jumla ya sh. trilioni 2.7 ambapo kati ya fedha hizo, sh. trilioni 2.4 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na sh. bilioni 230.3 kwa ajili ya kugharamia shughuli za maendeleo.

Na MUSSA YUSUPH, DODOMA

Abdurahman Jumanne

Abdurahman Jumanne

Stay Connected test

  • 114 Follower
  • 172k Subscriber
  • 23.6k Follower
  • 99 Subscriber
  • Trending
  • Comments
  • Latest
MADAKTARI WAELEZEA JINSI YA KUZUIA MIMBA ISIHARIBIKE

MADAKTARI WAELEZEA JINSI YA KUZUIA MIMBA ISIHARIBIKE

July 9, 2021
TABWA YAMSIFU SAMIA KUWAPA FURSA WANAWAKE

TABWA YAMSIFU SAMIA KUWAPA FURSA WANAWAKE

July 9, 2021
BEI MPYA YA MBAAZI, KUNDE YAWAPANDISHA MZUKA WAKULIMA

BEI MPYA YA MBAAZI, KUNDE YAWAPANDISHA MZUKA WAKULIMA

August 9, 2021
MBUNGE LINDI ATAKA VIJANA WAJISHUGHULISHE

MBUNGE LINDI ATAKA VIJANA WAJISHUGHULISHE

July 8, 2021
NDUGU MATATANI KUMSHAMBULIA, KUMJERUHI MWENZAO KISA NG’OMBE

NDUGU MATATANI KUMSHAMBULIA, KUMJERUHI MWENZAO KISA NG’OMBE

0
WAHANDISI WA HALMASHAURI WAMEKUA WAKIIKOSEA SERIKALI KWAKUTOA TAARIFA ZA UONGO

WAHANDISI WA HALMASHAURI WAMEKUA WAKIIKOSEA SERIKALI KWAKUTOA TAARIFA ZA UONGO

0

OFISA ELIMU, MHANDISI, MKUU WA SHULE WAKALIA ‘KUTI KAVU’

0
STENDI YA ZAMANI UBUNGO  KUJENGWA DEPO MABASI MWENDOKASI

STENDI YA ZAMANI UBUNGO KUJENGWA DEPO MABASI MWENDOKASI

0
MIAKA 30 YA VYAMA VINGI: CHANGAMOTO NA MUSTAKABALI KUSONGA MBELE

MIAKA 30 YA VYAMA VINGI: CHANGAMOTO NA MUSTAKABALI KUSONGA MBELE

July 1, 2022
WAWILI WADAKWA DAR TUHUMA ZA BIASHARA YA NGONO MTANDAONI

WAWILI WADAKWA DAR TUHUMA ZA BIASHARA YA NGONO MTANDAONI

June 28, 2022
WAJUE WATIKISA NYAVU BORA 2021/2022

WAJUE WATIKISA NYAVU BORA 2021/2022

June 28, 2022
ATOZWA FAINI 100,000 KISA KUIBA PUNDA WA BABA YAKE

ATOZWA FAINI 100,000 KISA KUIBA PUNDA WA BABA YAKE

June 28, 2022

Recent News

MIAKA 30 YA VYAMA VINGI: CHANGAMOTO NA MUSTAKABALI KUSONGA MBELE

MIAKA 30 YA VYAMA VINGI: CHANGAMOTO NA MUSTAKABALI KUSONGA MBELE

July 1, 2022
WAWILI WADAKWA DAR TUHUMA ZA BIASHARA YA NGONO MTANDAONI

WAWILI WADAKWA DAR TUHUMA ZA BIASHARA YA NGONO MTANDAONI

June 28, 2022
WAJUE WATIKISA NYAVU BORA 2021/2022

WAJUE WATIKISA NYAVU BORA 2021/2022

June 28, 2022
ATOZWA FAINI 100,000 KISA KUIBA PUNDA WA BABA YAKE

ATOZWA FAINI 100,000 KISA KUIBA PUNDA WA BABA YAKE

June 28, 2022
Instagram Youtube Twitter VK Facebook

We are a diverse team of experts, innovative thinkers, creative designers, writers, innovators, strategists, pyschologists, comunictaors and web developers. UMG is extremely passionate about growing clients’ businesses, helping them achieve their goals and making a difference by raising the creative and communications industry standards in Tanzania.

Follow Us

Browse by Category

  • 2021
  • Afya Makala
  • BURUDANI
  • Business
  • GAZETI LA BURUDANI
  • GAZETI LA UHURU
  • GAZETI LA UHURU MACHI 17
  • HABARI KIMATAIFA
  • Habari Kitaifa
  • Habari Picha
  • KIMATAIFA
  • MAKALA
  • MAKALA AFYA
  • MAKALA-BURUDANI
  • MICHEZO
  • MICHEZO KIMATAIFA
  • MICHEZO KITAIFA
  • MICHEZO-MAKALA
  • MICHEZO-MASUMBWI
  • MITINDO
  • RIWAYA
  • SIASA
  • Uncategorized

Recent News

MIAKA 30 YA VYAMA VINGI: CHANGAMOTO NA MUSTAKABALI KUSONGA MBELE

MIAKA 30 YA VYAMA VINGI: CHANGAMOTO NA MUSTAKABALI KUSONGA MBELE

July 1, 2022
WAWILI WADAKWA DAR TUHUMA ZA BIASHARA YA NGONO MTANDAONI

WAWILI WADAKWA DAR TUHUMA ZA BIASHARA YA NGONO MTANDAONI

June 28, 2022

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

No Result
View All Result

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In