Saturday, May 21, 2022
27 °c
Dar es Salaam
25 ° Thu
25 ° Fri
25 ° Sat
25 ° Sun
25 ° Mon
English EN Kiswahili SW
UHURU MEDIA GROUP
Tangaza Nasi
  • Mwanzo
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHAKA ANG’AKA FAINI MIMBA ZA WANAFUNZI

    NI HISTORIA NYINGINE CCM

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM YATEUA MAKATIBU WA MIKOA NA WILAYA

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM ITAENDELEA KUWA CHAMA BORA, IMARA AFRIKA- SHAKA

    MBISE ATOA VITI MIA MOJA MONDULI

    MBISE ATOA VITI MIA MOJA MONDULI

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
  • Michezo
    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    PABLO AIPANIA KMC 

    PABLO AIPANIA KMC 

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
  • UMG
    • Home
    • About Us
    • Services
    • Shop
    • Contact Us
  • MAGAZETI
    • Uhuru wanawake
    • Mzalendo
    • Uhuru vijijini
    • Burudani
    • Uhuru kijani
  • UHURU FM
    • Ratiba
  • UHURU DIGITAL
    • Instagram
    • Facebook
    • Twitter
    • Youtube
  • Mwanzo
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHAKA ANG’AKA FAINI MIMBA ZA WANAFUNZI

    NI HISTORIA NYINGINE CCM

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM YATEUA MAKATIBU WA MIKOA NA WILAYA

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM ITAENDELEA KUWA CHAMA BORA, IMARA AFRIKA- SHAKA

    MBISE ATOA VITI MIA MOJA MONDULI

    MBISE ATOA VITI MIA MOJA MONDULI

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
  • Michezo
    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    PABLO AIPANIA KMC 

    PABLO AIPANIA KMC 

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
No Result
View All Result
UHURU MEDIA GROUP
No Result
View All Result
Mwanzo Habari Kitaifa

RAIS SAMIA ANG’ARA TENA

>>Ripoti ya Benki ya dunia yaanika mwelekeo mzuri wa Tanzania, kiuchumi, kijamii chini ya uongozi wake

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
March 2, 2022
in Habari Kitaifa
0 0
0
RAIS SAMIA ANG’ARA TENA

RAIS Samia Suluhu Hassan

0
SHARES
48
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

BENKI ya Dunia (WB), imetangaza kupungua kwa kiwango cha umasikini nchini kutoka asilimia 27.1 mwaka 2020 hadi asilimia 27.0 mwaka 2021, huku ikipongeza juhudi za Rais Samia Suluhu Hassan, kuondoa matabaka ya jinsia katika fursa za maendeleo ambazo ni siasa, uchumi na jamii.

Huo ni mwendelezo wa mafanikio ya Rais Samia, ambapo tayari amekuwa akitajwa kuweka mazingira mazuri ya kisera katika biashara, kuimarisha diplomasia ya uchumi na mapambano ya kisayansi dhidi ya ugonjwa wa Uviko 19.

Mwenendo huo wa hali ya umasikini ilitolewa na Mkurugenzi wa WB kwa nchi za Tanzania, Malawi, Zambia na Zimbabwe, Dk. Mara Warwick, wakati wa uzinduzi wa Taarifa ya 17 ya Mwenendo wa Uchumi wa Tanzania, yenye kaulimbiu ya ‘Uwezeshaji wanawake: Kupanua ufikiaji wa rasilimali na fursa za uchumi’.

Dk.Mara alieleza hatua hiyo ni matokeo ya juhudi zilizochukuliwa katika kukabiliana na janga la Uviko-19,ikiwemo ya mpango wa chanjo kwa wananchi ambao umesababisha shughuli za uchumi kuendelea kuimarika nchini.

MWELEKEO WA GDP

Kuhusu mwelekeo wa ukuaji wa Pato la Taifa (GDP), Dk. Mara alisema sekta ya malazi na migahawa, madini na umeme zilichangia kuongezeka kwa kasi ya ukuaji wa pato hilo, kwa robo mwaka katika robo ya tatu ya mwaka jana.

Kwa mujibu wa Dk. Mara, juhudi nyingine zilizofanywa ni maboresho katika uzalishaji wa saruji, umeme, mikopo ya sekta binafsi, mauzo ya bidhaa na huduma nje ya nchi, uagizaji wa bidhaa zisizo za mafuta kutoka nje, mawasiliano ya simu, uhamaji na kuwasili kwa watalii.

“Kwa sababu ya maendeleo haya chanya, Benki ya Dunia inakadiria kiwango halisi cha ukuaji wa Pato la Taifa cha asilimia 4.3 na kiwango cha ukuaji wa Pato la Taifa cha asilimia 1.3 mwaka 2021, kufuatia kupungua kwa Pato la Taifa kwa asilimia 1.0 mwaka 2020,” alisema.

VITA DHIDI YA UVIKO

Aliishauri serikali kuimarisha mwitikio wake katika janga la Uviko-19, katika muda mfupi kwa kushirikiana na sekta binafsi katika muda wa kati hadi mrefu.

Aidha, Dk. Mara alifafanua kwamba hatari kwa mtazamo wa kiuchumi wa Tanzania zimepungua, lakini hilo litaimarika zaidi iwapo sekta binafsi itashirikishwa vyema.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkazi wa WB, mpango wa utoaji chanjo ya Covid-19 kwa wananchi umechochea kuongezeka kwa biashara, ushirikiano wa kikanda na mageuzi ya sera iliyoundwa kuboresha mazingira ya biashara na kusaidia ukuaji wa sekta ya binafsi.

Dk. Mara alisisitiza kuna umuhimu wa serikali kuimarisha juhudi katika kukabiliana na janga la Uviko-19, ili kuwezesha kuondolewa kwa vikwazo vya usafiri katika baadhi ya nchi na hatimaye sekta ya utalii kuimarika zaidi.

Aliongeza kwamba, taarifa hiyo inalenga kuwawezesha wanawake kiuchumi na kuongeza upatikanaji wa rasilimali za uzalishaji mali.

USAWA WA KIJINSIA

“Sasa ni wakati wa Tanzania kuchukua hatua, Rais Samia Suluhu Hassan, ameweka dira ya kimkakati yenye matarajio ya mbele kwa ajili ya kuwawezesha wanawake wa Tanzania. Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2025 pia inasisitiza usawa wa kijinsia katika nyanja zake za kijamii, kiuchumi na kisiasa,”alisema.

Alieleza kwa Tanzania ushiriki wa wanawake katika nguvu kazi umeongezeka kutoka asilimia 67 mwaka 2000, hadi asilimia 80 mwaka 2019, juu ya wastani wa asilimia 63 kwa Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara (SSA).

Dk. Mara alisema pamoja na juhudi zinazofanywa na serikali lakini bado, wanawake nchini wanakumbwa na vikwazo hasa katika upatikanaji wa ardhi na rasilimali, jambo ambalo linaathiri tija yao katika uchumi.

Alibainisha kwamba asilimia 25 ya wanaume nchini ndiyo wamiliki pekee wa ardhi, ikilinganishwa na asilimia nane ya wanawake, huku makadirio yakionyesha asilimia 42 ya wanawake nchini ndiyo wenye uwezo wa kuzifikia akaunti za benki, wakati wanaume ni asilimia 52.

“Inakadiriwa kuwa asilimia 22 ya wanawake wa Tanzania wanajishughulisha na ajira za ujira, ikilinganishwa na asilimia 48 ya wanaume. Kati ya wafanyakazi wanaolipwa mishahara wanawake hupata senti 88 pekee kwa kila dola inayopatikana kwa wanaume,” alisema.

Alisema hata katika sekta ya kilimo uzalishaji wa wanawake ni kati ya asilimia 20 na 30 tu, kutokana na kuwa na shughuli nyingi za kifamilia, kukosa zana za kilimo na pembejeo.

“Makadirio yanaonyesha kuwa kuziba pengo la kijinsia la masharti katika tija ya kilimo kunaweza kuwainua takriban Watanzania 80,000 kutoka katika umaskini kila mwaka huku kukiongeza pato la kilimo kwa mwaka kwa asilimia 2.7 na kukuza Pato la Taifa kwa asilimia 0.86,” alisema.

Ili kuimarisha uwezo wa wanawake, Dk. Mara alisema taarifa hiyo inapendekeza waboreshewe ujuzi kupitia fursa zilizopanuliwa za uanagenzi na programu za mafunzo.

Alitaja nyingine ni kuimarisha haki za ardhi za wanawake kwa kutoa ruzuku ya hati miliki ya ardhi kwa kaya na motisha ili kuwahimiza wanandoa kumiliki ardhi pamoja, kupanua uwezo wa wanawake kutumia pembejeo za kilimo, teknolojia za kidijitali ili kuboresha uzalishaji wa kilimo kwao.

Pia, alisema wanawake waimarishiwe uwezo wa kusimamia fedha zao za kibinafsi na za biashara, kukomesha ndoa za watoto, na kutoa usaidizi wa malezi ya watoto ili kuruhusu na kuhimiza ushiriki mkubwa wa wanawake katika nguvu kazi.

“Jambo jingine ni kutekeleza sheria zinazowalinda wanawake dhidi ya ukatili,” alisema.

Ripoti hiyo ni ya 17 kutolewa ambapo hutolewa kila baada ya miaka miwili, ikiangalia mambo mbalimbali, ambapo ripoti ya 16 iliangalia mageuzi ya kimfumo katika sekta ya utalii, ili iwe endelevu.

NA JUMA ISSIHAKA

Abdurahman Jumanne

Abdurahman Jumanne

Stay Connected test

  • 111 Follower
  • 168k Subscriber
  • 23.5k Follower
  • 99 Subscriber
  • Trending
  • Comments
  • Latest
MADAKTARI WAELEZEA JINSI YA KUZUIA MIMBA ISIHARIBIKE

MADAKTARI WAELEZEA JINSI YA KUZUIA MIMBA ISIHARIBIKE

July 9, 2021
TABWA YAMSIFU SAMIA KUWAPA FURSA WANAWAKE

TABWA YAMSIFU SAMIA KUWAPA FURSA WANAWAKE

July 9, 2021
BEI MPYA YA MBAAZI, KUNDE YAWAPANDISHA MZUKA WAKULIMA

BEI MPYA YA MBAAZI, KUNDE YAWAPANDISHA MZUKA WAKULIMA

August 9, 2021
MBUNGE LINDI ATAKA VIJANA WAJISHUGHULISHE

MBUNGE LINDI ATAKA VIJANA WAJISHUGHULISHE

July 8, 2021
JAFO AWATAKA WAKAZI WA MKOA WA MARA KUJIKITA KATIKA ZAO LA ALIZETI

JAFO AWATAKA WAKAZI WA MKOA WA MARA KUJIKITA KATIKA ZAO LA ALIZETI

0
KIHONGOSI : NGORONGORO MCHAGUENI SHANGAI

KIHONGOSI : NGORONGORO MCHAGUENI SHANGAI

0
JWTZ IKO IMARA KUKABILI MATUKIO YA KIGAIDI-SERIKALI

JWTZ IKO IMARA KUKABILI MATUKIO YA KIGAIDI-SERIKALI

0
MAJALIWA AANIKA SIRI UJENZI VYUO VYA VETA

MAJALIWA AANIKA SIRI UJENZI VYUO VYA VETA

0
MIPAKA YA TANZANIA IPO SHWARI

MIPAKA YA TANZANIA IPO SHWARI

May 20, 2022
SERIKALI YATOA KIPAUMBELE CHA AJIRA KWA WENYE ULEMAVU

SERIKALI YATOA KIPAUMBELE CHA AJIRA KWA WENYE ULEMAVU

May 20, 2022
RAIS SAMIA: MAWAZIRI CHAPENI KAZI, MSISIKILIZE MANENO

RAIS SAMIA: MAWAZIRI CHAPENI KAZI, MSISIKILIZE MANENO

May 20, 2022
TAKUKURU YAIVALIA NJUGA MIRADI ILIYOKATALIWA MBIO ZA MWENGE

TAKUKURU YAIVALIA NJUGA MIRADI ILIYOKATALIWA MBIO ZA MWENGE

May 18, 2022

Recent News

MIPAKA YA TANZANIA IPO SHWARI

MIPAKA YA TANZANIA IPO SHWARI

May 20, 2022
SERIKALI YATOA KIPAUMBELE CHA AJIRA KWA WENYE ULEMAVU

SERIKALI YATOA KIPAUMBELE CHA AJIRA KWA WENYE ULEMAVU

May 20, 2022
RAIS SAMIA: MAWAZIRI CHAPENI KAZI, MSISIKILIZE MANENO

RAIS SAMIA: MAWAZIRI CHAPENI KAZI, MSISIKILIZE MANENO

May 20, 2022
TAKUKURU YAIVALIA NJUGA MIRADI ILIYOKATALIWA MBIO ZA MWENGE

TAKUKURU YAIVALIA NJUGA MIRADI ILIYOKATALIWA MBIO ZA MWENGE

May 18, 2022
Instagram Youtube Twitter VK Facebook

We are a diverse team of experts, innovative thinkers, creative designers, writers, innovators, strategists, pyschologists, comunictaors and web developers. UMG is extremely passionate about growing clients’ businesses, helping them achieve their goals and making a difference by raising the creative and communications industry standards in Tanzania.

Follow Us

Browse by Category

  • 2021
  • Afya Makala
  • BURUDANI
  • Business
  • GAZETI LA BURUDANI
  • GAZETI LA UHURU
  • GAZETI LA UHURU MACHI 17
  • HABARI KIMATAIFA
  • Habari Kitaifa
  • Habari Picha
  • KIMATAIFA
  • MAKALA
  • MAKALA AFYA
  • MAKALA-BURUDANI
  • MICHEZO
  • MICHEZO KIMATAIFA
  • MICHEZO KITAIFA
  • MICHEZO-MAKALA
  • MICHEZO-MASUMBWI
  • MITINDO
  • RIWAYA
  • SIASA
  • Uncategorized

Recent News

MIPAKA YA TANZANIA IPO SHWARI

MIPAKA YA TANZANIA IPO SHWARI

May 20, 2022
SERIKALI YATOA KIPAUMBELE CHA AJIRA KWA WENYE ULEMAVU

SERIKALI YATOA KIPAUMBELE CHA AJIRA KWA WENYE ULEMAVU

May 20, 2022

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

No Result
View All Result

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In