Saturday, May 21, 2022
27 °c
Dar es Salaam
25 ° Thu
25 ° Fri
25 ° Sat
25 ° Sun
25 ° Mon
English EN Kiswahili SW
UHURU MEDIA GROUP
Tangaza Nasi
  • Mwanzo
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHAKA ANG’AKA FAINI MIMBA ZA WANAFUNZI

    NI HISTORIA NYINGINE CCM

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM YATEUA MAKATIBU WA MIKOA NA WILAYA

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM ITAENDELEA KUWA CHAMA BORA, IMARA AFRIKA- SHAKA

    MBISE ATOA VITI MIA MOJA MONDULI

    MBISE ATOA VITI MIA MOJA MONDULI

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
  • Michezo
    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    PABLO AIPANIA KMC 

    PABLO AIPANIA KMC 

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
  • UMG
    • Home
    • About Us
    • Services
    • Shop
    • Contact Us
  • MAGAZETI
    • Uhuru wanawake
    • Mzalendo
    • Uhuru vijijini
    • Burudani
    • Uhuru kijani
  • UHURU FM
    • Ratiba
  • UHURU DIGITAL
    • Instagram
    • Facebook
    • Twitter
    • Youtube
  • Mwanzo
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHAKA ANG’AKA FAINI MIMBA ZA WANAFUNZI

    NI HISTORIA NYINGINE CCM

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM YATEUA MAKATIBU WA MIKOA NA WILAYA

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM ITAENDELEA KUWA CHAMA BORA, IMARA AFRIKA- SHAKA

    MBISE ATOA VITI MIA MOJA MONDULI

    MBISE ATOA VITI MIA MOJA MONDULI

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
  • Michezo
    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    PABLO AIPANIA KMC 

    PABLO AIPANIA KMC 

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
No Result
View All Result
UHURU MEDIA GROUP
No Result
View All Result
Mwanzo Habari Kitaifa

SHAKA ATAJA MAFANIKIO LUKUKI MIAKA 45 YA CCM

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
February 5, 2022
in Habari Kitaifa
0 0
0
SHAKA: WAPIGANIA VYEO HAWAWEZI KUTUYUMBISHA

Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Shaka Hamdu Shaka

0
SHARES
59
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

KATIBU wa NEC, Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Shaka Hamdu Shaka, amesema katika kipindi cha miaka 45 tangu kuzaliwa kwa CCM, Chama kimekuwa kinara kwa kuchochea mageuzi ya demokrasia Afrika kwa kuendelea kupiga vita siasa chafu zenye mrengo wa ubaguzi.

Amesisitiza CCM itaendelea kuwa Chama sikivu, makini na kujali dhima ya majadiliano kwa njia za kiungwana kuliko kuandamwa na vitisho, kebehi, ubabe au kushurutishwa.

Akizungumza na waandishi wa habari wilayani Musoma, Mkoa wa Mara kuhusu mafanikio ya chama hicho kikongwe barani Afrika, ndani ya miaka 45 tangu kilipozaliwa baada ya kuungana vyama vya TANU na Afro-Shiraz Party (ASP), mwaka 1977, alisema kuwa,

CCM iko tayari kupokea maoni, ushauri na maafikiano yanayoheshimu njia za kiungwana na kistaarabu kwa maslahi mapana ya Taifa.

“Kazi kubwa ya utekelezaji wa  sera kwa miaka yote ya utawala wa  CCM madarakani ni kuhakikisha umoja  wa kitaifa,  unadumu na kubaki tukipinga  siasa chafu  za  ukabila, rangi, dini au  ukanda badala yake, sera zake zimekuwa zikihimiza umoja  na mshikamano, hali ambayo imelifanya Taifa letu kuwa lenye utulivu, upendo na ushirikiano,” alisema.

MAFANIKIO YA CCM MIAKA 45

Akizungumzia mafanikio ambayo CCM inajivunia tangu kuzaliwa kwake, Shaka alisema kwamba, katika kipindi hicho, Chama kimeendelea kuwaongoza Watanzania katika kulinda uhuru wa nchi yao na harakati za kujiletea maendeleo yao.

Alisema mafanikio ya dhahiri, yameonekana kupitia utekelezaji wa sera zake mbalimbali na kujijengea uhalali wa kuongoza nchi katika dunia ya sasa yenye mazingira yanayobadilika kila mara.

“Moja ya mafanikio makubwa yaliyopatikana ni kudumu na kuimarika kwa muungano wetu. Katika kipindi cha miaka 45 iliyopita, muungano wetu umezidi kuimarika kutokana na juhudi za makusudi za chama chetu kuhakikisha muungano wetu unadumu milele.

“Tumefanikiwa kutatua changamoto mbalimbali ziliyojitokeza katika muungano wetu.

Aliongeza kuwa: “Tumeweza kufanya mambo kadhaa mapya ambayo yamefanya mambo yaende vizuri zaidi. Kitendo cha kuungana kwa TANU na ASP, ndiyo kilichozaa chombo kilichokuwa na nguvu na uwezo mkubwa zaidi wa kukabiliana na changamoto za muungano wetu.”

Alibainisha kwa sasa, muungano umekuwa mfano bora wa kuigwa si barani Afrika pekee, isipokuwa duniani kote ambapo Watanzania wameudhihirishia Ulimwengu kuwa, dhamira ya kuungana ni imara na haitetereki.

“Tutaendelea kuimarisha muungano wetu kwa faida ya nchi yetu na watu wetu. Tunafanya hivyo kwa kutambua faida kubwa na nyingi zinazotokana na muungano wetu ambazo kila mmoja wetu anazitambua,” alisema.

 UMOJA WA KITAIFA

Shaka alieleza kuwa, mafanikio mengine ambayo chama kinajivunia ni kuimarisha umoja wa kitaifa kama ilivokuwa kwa vyama vya TANU na ASP, sera za CCM zimeendelea kulenga katika kuwaunganisha Watanzania na kujenga taifa moja imara lenye watu wamoja.

Alisema licha ya tofauti za kisiasa, rangi, dini au kabila, kila mmoja anajivunia na kuona faraja kuwa Mtanzania na kuendelea kuimarisha amani, utulivu na mshikamano, mambo ambayo baadhi ya mataifa ya Afrika na duniani ni bidhaa adimu.

 “Tumeweza kufanikiwa kubaki kuwa na taifa lenye umoja na utulivu, licha ya nchi yetu kupitia katika kipindi kigumu cha mageuzi ya kisiasa na kiuchumi na kuingia katika mfumo wa vyama vingi na uchumi wa soko huria. Licha ya umoja wetu hata ukomavu wa kisiasa wa wananchi wetu, pia umeimarika.

“Watanzania ni watu wasioyumba wala kubabaishwa. Ni watu makini, wachambuzi na watambuzi mahiri.

“Haya ni mafanikio makubwa, ni jambo la kujivunia. Lakini ni sifa kubwa kwa chama chetu ambacho ndicho kiliongoza mageuzi hayo nchini.

“CCM itaendelea kuimarisha dhamira yetu ya kudumisha na kuendeleza umoja, amani na utulivu wa taifa letu,” alifafanua.

 HUDUMA ZA JAMII

Kwa mujibu wa Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, taifa limepiga hatua hatua na kupata mafanikio mbalimbali katika nyanja za kiuchumi na kijamii.

“Pamoja na kuwa bado nchi yetu ni maskini, hali za watu wetu ni bora zaidi sasa kuliko ilivyokuwa mwaka 1977. Watu wengi wana kipato kikubwa, wanaishi katika nyumba bora zaidi, wanavaa vizuri na wanakula vizuri.

“Utoaji wa huduma za elimu, huduma za afya, maji, barabara, umeme zimeimarika kuliko ilivyokuwa huko nyuma. Haya yote yanatokana na sera sahihi na mipango mizuri ya Chama Cha Mapinduzi.

MWALIMU WA DEMOKRASIA

Kuhusu demokrasia, alieleza kuwa, CCM imekuwa mwalimu wa Demokrasia nchini, mataifa jirani na kimeweza kusimamia na kuongoza nchi kufanya uchaguzi, wananchi kutumia mamlaka na haki zao za kikatiba kuchagua viongozi wanaowataka kwa amani na Utulivu.

Aidha, alisema CCM ndani ya miaka 45, imefanikiwa kusimamia muundo wa sera, mikakati na aina ya siasa inayohitajika katika nyakati za sasa, jambo lililosaidia kulinda na kusimamia usalama wa taifa na watu wake ili kudumisha amani, umoja na kujivunia uhuru wake.

Alisema kazi kubwa ya utekelezaji wa  sera kwa miaka yote ya utawala wa CCM madarakani ni kuhakikisha umoja  wa kitaifa unadumu na kubaki kupinga  siasa chafu za ukabila, rangi, dini au  ukanda badala yake, sera zake zimekuwa zikihimiza umoja  na mshikamano hali ambayo imelifanya taifa kuwa lenye utulivu, upendo na ushirikiano.

“Katika nyakati zote, kila mwananchi amekuwa mlinzi wa Taifa lake, askari wa mstari wa mbele anayehakikisha hatokei adui akayejivisha koti la kuwa kibaraka au wakala, badala yake mapambano yameelekezwa dhidi ya maadui ujinga, umasikini na maradhi,” alisisitiza.

USHIRIKIANO KISIASA

Shaka alisema kwa miaka yote 45, CCM imekuwa mstari  wa mbele kuendeleza na kudumisha ujirani mwema ili kujenga haiba ya maendeleo ya kisiasa, kijamii, kiuchumi, kudumisha uhusiano mwema, kuendeleza ushirikiano na vyama vingine rafiki na vya kidugu duniani ikiwemo kanda ya Afrika Mashariki.

Alieleza CCM, imeendeleza mahusiano hayo ili kuhakikisha ujirani mwema unadumu, unaendelezwa kwa kuwaletea manufaa wananchi wa Tanzania na mataifa mengine.

Vilevile, alisema CCM katika kipindi cha miaka 45, imekuwa chachu ya kuanzishwa kwa kamati ya nchi tano zilizo mstari wa mbele kusini mwa Afrika, kipindi ambacho mataifa kadhaa yalikuwa bado hayajapata uhuru.

Kwa kushirikiana na vyama vingine vya ukombozi, CCM kimekuwa na mchango kwa mataifa hayo kushamirisha juhudi za ukombozi hadi mataifa hayo yalipopata uhuru na kujitawala yenyewe.

“Dhana ya mfumo  wa demokrasia ya vyama vingi ni kutanuka kwa wigo wa demokrasia shirikishi, ushindani wa sera kwa sera, ujenzi wa hoja kwa nguvu ya hoja. Kwa kipindi chote cha miaka 45 CCM kimeendelea kuwa Chama sikivu na makini kwa nyakati zote.

“Kinapenda na kujali dhima ya majadiliano kwa njia za kiungwana kuliko kuandamwa na vitisho, kebehi, ubabe au kushuritishwa. CCM kipo tayari wakati wote kupokea maoni, ushauri na rai hatimaye kufikia kwa maafikiano yanayoheshimu njia za kiungwana na kistaarabu kwa maslahi mapana ya taifa letu,” Shaka alieleza.

Alitoa wito kwa Watanzania kuendeleza umoja, mshikamno wa taifa na kuendelea kuvisihi na kuviomba vyama vyote vya siasa nchini kuendeleze umoja wa kitaifa, kuthamini na kukuza ustawi wa demokrasia iliopo nchini.

Alisema yapo mataifa mengi duniani hivi sasa yanatamani yafanane na Tanzania lakini kwa bahati mbaya haiwezekani baada ya baadhi ya wanasiasa wao kuvuruga amani yao.

Shaka alisema mafanikio hayo yamekuwa msukumo mkubwa wa ujenzi wa imani kwa wananchi wa Tanzania na imani hiyo itaendelea kulindwa na kuheshimiwa kwa utiifu.

“Kwa namna ya pekee Chama Cha Mapinduzi kinamshukuru na kumpongeza Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Samia Suluhu Hassan kwa namna alivyojipambanua tangu alipochukua hatamu ya uongozi wa kuliongoza taifa kwani ameonyesha uwezo, juhudi na jinsi alivyodhamiria kukabiliana dhidi ya changamoto mbalimbali za kiuchumi, kijamii na kisiasa katika kusukuma maendeleo endelevu ya nchi yetu,” Shaka alieleza.

NA MUSSA YUSUPH, MUSOMA

Abdurahman Jumanne

Abdurahman Jumanne

Stay Connected test

  • 111 Follower
  • 168k Subscriber
  • 23.5k Follower
  • 99 Subscriber
  • Trending
  • Comments
  • Latest
MADAKTARI WAELEZEA JINSI YA KUZUIA MIMBA ISIHARIBIKE

MADAKTARI WAELEZEA JINSI YA KUZUIA MIMBA ISIHARIBIKE

July 9, 2021
TABWA YAMSIFU SAMIA KUWAPA FURSA WANAWAKE

TABWA YAMSIFU SAMIA KUWAPA FURSA WANAWAKE

July 9, 2021
BEI MPYA YA MBAAZI, KUNDE YAWAPANDISHA MZUKA WAKULIMA

BEI MPYA YA MBAAZI, KUNDE YAWAPANDISHA MZUKA WAKULIMA

August 9, 2021
MBUNGE LINDI ATAKA VIJANA WAJISHUGHULISHE

MBUNGE LINDI ATAKA VIJANA WAJISHUGHULISHE

July 8, 2021
JAFO AWATAKA WAKAZI WA MKOA WA MARA KUJIKITA KATIKA ZAO LA ALIZETI

JAFO AWATAKA WAKAZI WA MKOA WA MARA KUJIKITA KATIKA ZAO LA ALIZETI

0
KIHONGOSI : NGORONGORO MCHAGUENI SHANGAI

KIHONGOSI : NGORONGORO MCHAGUENI SHANGAI

0
JWTZ IKO IMARA KUKABILI MATUKIO YA KIGAIDI-SERIKALI

JWTZ IKO IMARA KUKABILI MATUKIO YA KIGAIDI-SERIKALI

0
MAJALIWA AANIKA SIRI UJENZI VYUO VYA VETA

MAJALIWA AANIKA SIRI UJENZI VYUO VYA VETA

0
MIPAKA YA TANZANIA IPO SHWARI

MIPAKA YA TANZANIA IPO SHWARI

May 20, 2022
SERIKALI YATOA KIPAUMBELE CHA AJIRA KWA WENYE ULEMAVU

SERIKALI YATOA KIPAUMBELE CHA AJIRA KWA WENYE ULEMAVU

May 20, 2022
RAIS SAMIA: MAWAZIRI CHAPENI KAZI, MSISIKILIZE MANENO

RAIS SAMIA: MAWAZIRI CHAPENI KAZI, MSISIKILIZE MANENO

May 20, 2022
TAKUKURU YAIVALIA NJUGA MIRADI ILIYOKATALIWA MBIO ZA MWENGE

TAKUKURU YAIVALIA NJUGA MIRADI ILIYOKATALIWA MBIO ZA MWENGE

May 18, 2022

Recent News

MIPAKA YA TANZANIA IPO SHWARI

MIPAKA YA TANZANIA IPO SHWARI

May 20, 2022
SERIKALI YATOA KIPAUMBELE CHA AJIRA KWA WENYE ULEMAVU

SERIKALI YATOA KIPAUMBELE CHA AJIRA KWA WENYE ULEMAVU

May 20, 2022
RAIS SAMIA: MAWAZIRI CHAPENI KAZI, MSISIKILIZE MANENO

RAIS SAMIA: MAWAZIRI CHAPENI KAZI, MSISIKILIZE MANENO

May 20, 2022
TAKUKURU YAIVALIA NJUGA MIRADI ILIYOKATALIWA MBIO ZA MWENGE

TAKUKURU YAIVALIA NJUGA MIRADI ILIYOKATALIWA MBIO ZA MWENGE

May 18, 2022
Instagram Youtube Twitter VK Facebook

We are a diverse team of experts, innovative thinkers, creative designers, writers, innovators, strategists, pyschologists, comunictaors and web developers. UMG is extremely passionate about growing clients’ businesses, helping them achieve their goals and making a difference by raising the creative and communications industry standards in Tanzania.

Follow Us

Browse by Category

  • 2021
  • Afya Makala
  • BURUDANI
  • Business
  • GAZETI LA BURUDANI
  • GAZETI LA UHURU
  • GAZETI LA UHURU MACHI 17
  • HABARI KIMATAIFA
  • Habari Kitaifa
  • Habari Picha
  • KIMATAIFA
  • MAKALA
  • MAKALA AFYA
  • MAKALA-BURUDANI
  • MICHEZO
  • MICHEZO KIMATAIFA
  • MICHEZO KITAIFA
  • MICHEZO-MAKALA
  • MICHEZO-MASUMBWI
  • MITINDO
  • RIWAYA
  • SIASA
  • Uncategorized

Recent News

MIPAKA YA TANZANIA IPO SHWARI

MIPAKA YA TANZANIA IPO SHWARI

May 20, 2022
SERIKALI YATOA KIPAUMBELE CHA AJIRA KWA WENYE ULEMAVU

SERIKALI YATOA KIPAUMBELE CHA AJIRA KWA WENYE ULEMAVU

May 20, 2022

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

No Result
View All Result

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In