Wednesday, May 18, 2022
27 °c
Dar es Salaam
25 ° Thu
25 ° Fri
25 ° Sat
25 ° Sun
25 ° Mon
English EN Kiswahili SW
UHURU MEDIA GROUP
Tangaza Nasi
  • Mwanzo
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHAKA ANG’AKA FAINI MIMBA ZA WANAFUNZI

    NI HISTORIA NYINGINE CCM

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM YATEUA MAKATIBU WA MIKOA NA WILAYA

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM ITAENDELEA KUWA CHAMA BORA, IMARA AFRIKA- SHAKA

    MBISE ATOA VITI MIA MOJA MONDULI

    MBISE ATOA VITI MIA MOJA MONDULI

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
  • Michezo
    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    PABLO AIPANIA KMC 

    PABLO AIPANIA KMC 

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
  • UMG
    • Home
    • About Us
    • Services
    • Shop
    • Contact Us
  • MAGAZETI
    • Uhuru wanawake
    • Mzalendo
    • Uhuru vijijini
    • Burudani
    • Uhuru kijani
  • UHURU FM
    • Ratiba
  • UHURU DIGITAL
    • Instagram
    • Facebook
    • Twitter
    • Youtube
  • Mwanzo
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHAKA ANG’AKA FAINI MIMBA ZA WANAFUNZI

    NI HISTORIA NYINGINE CCM

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM YATEUA MAKATIBU WA MIKOA NA WILAYA

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM ITAENDELEA KUWA CHAMA BORA, IMARA AFRIKA- SHAKA

    MBISE ATOA VITI MIA MOJA MONDULI

    MBISE ATOA VITI MIA MOJA MONDULI

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
  • Michezo
    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    PABLO AIPANIA KMC 

    PABLO AIPANIA KMC 

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
No Result
View All Result
UHURU MEDIA GROUP
No Result
View All Result
Mwanzo MICHEZO KITAIFA

SULUHISHO LA MATATIZO YALIYOPO YANGA NI KUBADILI MFUMO WA UENDESHAJI WA KLABU

WAZO LA WIKI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
March 15, 2021
in MICHEZO KITAIFA
0 0
0
SULUHISHO LA MATATIZO YALIYOPO YANGA NI KUBADILI MFUMO WA UENDESHAJI WA KLABU
0
SHARES
382
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na Rashid Zahor

JUNI 15, mwaka jana, klabu kongwe ya Yanga iliandaa hafla maalumu na ya kihistoria, iliyopewa jina la ‘Kubwa Kuliko’, lengo lake kubwa likiwa kutoa nafasi kwa wanachama na wadau kuichangia timu hiyo.

Katika hafla hiyo, Yanga ilifanikiwa kupata zaidi ya sh. milioni 600, zilizotokana na michango ya fedha taslimu na ahadi kutoka kwa wadau mbalimbali, zikiwemo kampuni zinazojihusisha kwa karibu na michezo nchini.

Kuandaliwa kwa hafla hiyo kulitokana na ukweli kwamba, Yanga ilikuwa na hali mbaya kifedha, ikiwa ni pamoja na kudaiwa mamilioni ya fedha na wachezaji wake, zikiwemo malimbikizo ya mishahara na fedha za usajili.

Vilevile, Yanga ilikuwa ikikabiliwa na ukosefu wa fedha kwa ajili ya kusajili wachezaji wapya na kuwaongezea mikataba mipya wale wa zamani, hali iliyosababisha viongozi kubuni tukio hilo ili kupata fedha za kutatua matatizo hayo.

Akizungumza katika tukio hilo, Rais mstaafu wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete, ambaye alikuwa mgeni rasmi, aliamua kuweka wazi mambo mengi kuhusu maendeleo ya mchezo wa soka nchini, uendeshaji wake na pia kushauri njia za kuikwamua klabu hiyo kutoka katika matatizo iliyonayo sasa.

Miongoni mwa ushauri alioutoa ni kuitaka Yanga kubuni mfumo mpya wa kuiendesha klabu hiyo kisasa, ikiwa ni pamoja na kuwekeza katika soka ya vijana kwa lengo la kuwaandaa wachezaji wa baadaye wa timu hiyo.

Rais huyo mstaafu, alisema mazoea yaliyojengeka hivi sasa kwa klabu za Tanzania, hasa Simba, Yanga na Azam, kusajili wachezaji wengi wa kigeni, badala ya wale wa ndani, yanachangia kwa kiasi kikubwa kuzorotesha maendeleo ya mchezo huo kwa timu ya Taifa, Taifa Stars na pia kufifisha vipaji vya vijana.

Nimeikumbuka hotuba hiyo ya Rais mstaafu Kikwete katika hafla hiyo, kufuatia hali ya sintofahamu iliyoibuka hivi karibuni, baada ya uongozi wa Yanga, chini ya Mwenyekiti Mshindo Msolla, kutangaza kulivunja benchi lote la ufundi lililokuwa chini ya Kocha Mkuu, Cedrick Kaze.

Uamuzi wa Yanga kulivunja benchi la ufundi na kumfungashia virago Kaze, umekuja kwa kile kinachodaiwa timu hiyo kuanza vibaya mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara, hasa baada ya kufungwa mabao 2-1 na Coastal Union mjini Tanga na kulazimishwa kutoka sare ya bao 1-1 na Polisi Tanzania mjini Arusha.

Matokeo hayo yamepunguza pengo la pointi kati ya Yanga na watani wao wa jadi Simba, ambao baada ya nao kulazimishwa kutoka sare ya bao 1-1 na Prisons mjini Dar es Salaam, watakuwa na uwezo wa kuipiku Yanga kwa tofauti ya pointi tano, iwapo watashinda mechi zao zote za viporo zilizosalia.

 

Yanga, imemtimua Kaze, raia wa Burundi, ikiwa ni miezi sita tangu alipoanza kuinoa timu hiyo, akiwa ameiongoza katika mechi 18, imeshinda 10, kutoka sare saba na kufungwa moja.

Klabu hiyo imeamua kumrejesha aliyekuwa Kocha Msaidizi, Juma Mwambusi, ambaye aliomba kupumzika kwa madai ya afya yake kuwa siyo nzuri.

Mbali na Mwambusi, uongozi wa Yanga pia umeamua kumrejesha kocha wake wa viungo,

Edem Mortotsi kutoka Ghana, ambaye alikuwa sehemu ya benchi la ufundi lililovunjwa.

Mghana huyo pamoja na Mwambusi wapo kambini na timu hiyo hivi sasa.

Uamuzi wa Yanga kumrejesha Mwambusi katika nafasi yake, umeacha maswali mengi. Wadau wengi wa soka nchini wamekuwa wakijiuliza iwapo ni kweli kocha huyo aliamua kupumzika kwa sababu za kiafya ama hakuwa akielewana na Kaze. Hiyo ni siri ya Mwambusi na Kaze.

Licha ya Yanga kumrejesha Mwambusi katika nafasi yake ya awali, imeshaweka wazi kuhusu mipango yake ya kulisuka upya benchi la ufundi, kwa kumleta kocha mkuu mpya kutoka nje ya nchi. Bado haijafahamika jina la kocha huyo na nchi anakotoka.

Hii si mara ya kwanza kwa Yanga kuvunja benchi lake lote la ufundi. Iliwahi kufanya hivyo ilipokuwa chini ya Kocha Luc Eymael, aliyefukuzwa msimu uliopita, sanjari na aliyekuwa Kocha Msaidizi, Charles Boniface, aliyeamua kupumzika, Kocha wa Makipa, Peter Manyika, Meneja wa timu, Abeid Mziba na mtunza vifaa Fred Mbuna.

Pia, ilitangaza kuwaacha wachezaji 14, kutokana na sababu mbalimbali, ikiwemo kumaliza mikataba na wengine wakidaiwa kuwa ni utovu wa nidhamu. Wachezaji walioachwa ni nahodha Papy Tshishimbi, David Molinga, Mrisho Ngasa, Jaffar Mohamed, Tariq Seif, Andrew Vicent na Mohamed Issa. Pia, wapo waliositishiwa mikataba yao, Ali Mtoni, Muharami Issa, Ali Ali, Patrick Sibomana, Eric Kabamba, Rafael Daud na Yikpe Gislain.

Kilichodhihirika hadi sasa ni kwamba, pamoja na Yanga kusajili wachezaji kadhaa wapya na kubadili benchi la ufundi mara kwa mara, bado timu hiyo haijaweza kucheza katika mfumo unaoeleweka, badala yake kila mchezaji amekuwa akionyesha kipaji chake binafsi. Licha ya kuongoza ligi kwa muda mrefu, bado mashabiki hawajaridhishwa na kiwango cha soka kinachoonyeshwa na timu hiyo katika mechi zake.

Kibaya zaidi, mashabiki wa Yanga hawana subira na timu yao, hasa inapoteleza katika baadhi ya mechi. Ni wepesi wa kususa na kuishia kutoa lawama kwa viongozi na wachezaji, badala ya kuendelea kutoa hamasa kwa timu yao.

Ikumbukwe kuwa kikosi cha sasa cha Yanga kinaundwa na wachezaji wengi wapya waliosajiliwa msimu huu, hivyo kinahitaji kupata muda mrefu wa mafunzo ili waweze kucheza kwa uelewano na soka ya kuvutia. Katika hilo, maandalizi hayapaswi kuwa ya kulipua, yanahitaji muda wa kutosha na yawe ya kitaalamu.

Ni kosa kubwa kwa mashabiki wa Yanga kulazimisha timu yao icheze kama Simba, inayoshiriki katika hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa Afrika. Ni kwa sababu kikosi cha Simba kimedumu pamoja kwa zaidi ya miaka mitatu na kiwango cha wachezaji wake wengi kipo juu ikilinganishwa na Yanga.

Ili kukabiliana vyema na matatizo yanayoikabili sasa Yanga, huu ni wakati mwafaka kwa klabu hiyo kutekeleza kwa vitendo ushauri uliotolewa na Rais mstaafu Kikwete, kuwataka viongozi wake wabuni mfumo mpya wa uendeshaji ili iweze kujitegemea, badala ya kutegemea zaidi misaada ya wafadhili.

Japokuwa kwa sasa Yanga ipo chini ya udhamini wa Kampuni ya GSM, kumekuwepo na mgongano na mwingiliano mkubwa katika utekelezaji wa majukumu ya klabu. Baadhi ya wakati, viongozi wa GSM wamekuwa wakifanyakazi zinazopaswa kufanywa na viongozi, hivyo kuwafanya waonekane kama mapambo.

Vilevile, Yanga imekuwa ikipitia kipindi kigumu hivi sasa kutokana na kukosa mapato ya uhakika, hali inayosababisha iendeshwe kwa kutegemea michango ya wanachama na baadhi ya wafadhili. Katika hali hii, ni vigumu kuwashawishi mashabiki wafurike uwanjani kuishangilia kwa sababu hawana uhakika na uwezo wa timu yao.

Ili mashabiki wavutike kufika uwanjani, lazima timu iwe na wachezaji wengi wazuri na wenye kiwango cha hali ya juu, wanaolipwa mishahara kwa wakati na kukamilishiwa fedha za usajili bila kuwepo ‘bla bla’ yoyote.

Hapa ndipo ninapoukumbuka ushauri uliotolewa na Rais mstaafu Kikwete, kwa viongozi na wanachama wa Yanga kwamba, lazima wabadilike kwa kubuni mfumo mpya na wa kisasa wa kiundeshaji ili iweze kujitegemea na kuacha kutegemea michango ya wanachama na wafadhili.

Mabadiliko hayo yanapaswa kuanza mapema kwa uongozi uliopo madarakani kuhakiki idadi ya wanachama wake kote nchini, ili kujua rasilimali watu iliyonayo na kisha kuhakiki mali za klabu kwa lengo la kujua thamani yake na hatimaye kugeuzwa kuwa mtaji.

Pengine siyo vibaya kwa Yanga kuwaiga wenzao wa Simba, kubadili katiba ya klabu hiyo ili iruhusu kuwepo kwa kampuni, ambayo itakuwa chini ya wawekezaji watakaomiliki hisa nyingi, kwa kufuata maelekezo yaliyotolewa na serikali, huku wanachama nao wakiruhusiwa kununua hisa kupitia kiwango watakachowekewa.

Kutokana na mabadiliko ya nyakati yalivyo hivi sasa, mpango uliokuwepo awali wa kuikodisha klabu kwa mwekezaji ama mfanyabiashaya yeyote haufai, kwani unaweza kusababisha mgogoro wa kimaslahi. Kwa kuwa klabu ni mali ya wanachama, njia pekee nzuri ni kuunda kampuni na iendeshwe kwa mfumo wa kununua hisa.

Abdurahman Jumanne

Abdurahman Jumanne

Stay Connected test

  • 110 Follower
  • 168k Subscriber
  • 23.5k Follower
  • 99 Subscriber
  • Trending
  • Comments
  • Latest
MADAKTARI WAELEZEA JINSI YA KUZUIA MIMBA ISIHARIBIKE

MADAKTARI WAELEZEA JINSI YA KUZUIA MIMBA ISIHARIBIKE

July 9, 2021
TABWA YAMSIFU SAMIA KUWAPA FURSA WANAWAKE

TABWA YAMSIFU SAMIA KUWAPA FURSA WANAWAKE

July 9, 2021
BEI MPYA YA MBAAZI, KUNDE YAWAPANDISHA MZUKA WAKULIMA

BEI MPYA YA MBAAZI, KUNDE YAWAPANDISHA MZUKA WAKULIMA

August 9, 2021
MBUNGE LINDI ATAKA VIJANA WAJISHUGHULISHE

MBUNGE LINDI ATAKA VIJANA WAJISHUGHULISHE

July 8, 2021
DK. MWINYI ASISITIZA UIMARA WA UCHUMI

DK. MWINYI ASISITIZA UIMARA WA UCHUMI

0
MAJALIWA AANIKA SIRI UJENZI VYUO VYA VETA

MAJALIWA AANIKA SIRI UJENZI VYUO VYA VETA

0
RAIS MUSEVENI AKAMILISHA ZIARA YAKE NCHINI

RAIS MUSEVENI AKAMILISHA ZIARA YAKE NCHINI

0
USWISI KUENDELEA KUIMARISHA UHUSIANO TANZANIA

USWISI KUENDELEA KUIMARISHA UHUSIANO TANZANIA

0
TAKUKURU YAIVALIA NJUGA MIRADI ILIYOKATALIWA MBIO ZA MWENGE

TAKUKURU YAIVALIA NJUGA MIRADI ILIYOKATALIWA MBIO ZA MWENGE

May 18, 2022
VIKUNDI VILIVYOPATA MIKOPO YA BILIONI 4/- VYAITWA TAKUKURU

VIKUNDI VILIVYOPATA MIKOPO YA BILIONI 4/- VYAITWA TAKUKURU

May 18, 2022
SHAKA AZIAGIZA WIZARA TATU MISITU YA HIFADHI

SHAKA AZITAKA TAASISI ZA UMMA NCHINI KUTENGA BAJETI ZA MIRADI

May 18, 2022
WIZARA YAANIKA MKAKATI MPYA KUKABILI BEI YA MBOLEA, MAFUTA

WIZARA YAANIKA MKAKATI MPYA KUKABILI BEI YA MBOLEA, MAFUTA

May 18, 2022

Recent News

TAKUKURU YAIVALIA NJUGA MIRADI ILIYOKATALIWA MBIO ZA MWENGE

TAKUKURU YAIVALIA NJUGA MIRADI ILIYOKATALIWA MBIO ZA MWENGE

May 18, 2022
VIKUNDI VILIVYOPATA MIKOPO YA BILIONI 4/- VYAITWA TAKUKURU

VIKUNDI VILIVYOPATA MIKOPO YA BILIONI 4/- VYAITWA TAKUKURU

May 18, 2022
SHAKA AZIAGIZA WIZARA TATU MISITU YA HIFADHI

SHAKA AZITAKA TAASISI ZA UMMA NCHINI KUTENGA BAJETI ZA MIRADI

May 18, 2022
WIZARA YAANIKA MKAKATI MPYA KUKABILI BEI YA MBOLEA, MAFUTA

WIZARA YAANIKA MKAKATI MPYA KUKABILI BEI YA MBOLEA, MAFUTA

May 18, 2022
Instagram Youtube Twitter VK Facebook

We are a diverse team of experts, innovative thinkers, creative designers, writers, innovators, strategists, pyschologists, comunictaors and web developers. UMG is extremely passionate about growing clients’ businesses, helping them achieve their goals and making a difference by raising the creative and communications industry standards in Tanzania.

Follow Us

Browse by Category

  • 2021
  • Afya Makala
  • BURUDANI
  • Business
  • GAZETI LA BURUDANI
  • GAZETI LA UHURU
  • GAZETI LA UHURU MACHI 17
  • HABARI KIMATAIFA
  • Habari Kitaifa
  • Habari Picha
  • KIMATAIFA
  • MAKALA
  • MAKALA AFYA
  • MAKALA-BURUDANI
  • MICHEZO
  • MICHEZO KIMATAIFA
  • MICHEZO KITAIFA
  • MICHEZO-MAKALA
  • MICHEZO-MASUMBWI
  • MITINDO
  • RIWAYA
  • SIASA
  • Uncategorized

Recent News

TAKUKURU YAIVALIA NJUGA MIRADI ILIYOKATALIWA MBIO ZA MWENGE

TAKUKURU YAIVALIA NJUGA MIRADI ILIYOKATALIWA MBIO ZA MWENGE

May 18, 2022
VIKUNDI VILIVYOPATA MIKOPO YA BILIONI 4/- VYAITWA TAKUKURU

VIKUNDI VILIVYOPATA MIKOPO YA BILIONI 4/- VYAITWA TAKUKURU

May 18, 2022

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

No Result
View All Result

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In