Saturday, July 2, 2022
27 °c
Dar es Salaam
25 ° Thu
25 ° Fri
25 ° Sat
25 ° Sun
25 ° Mon
English EN Kiswahili SW
UHURU MEDIA GROUP
Tangaza Nasi
  • Mwanzo
  • Siasa
    • All
    • Business
    MEMBE ATOA YA MOYONI AKIREJEA CCM

    MEMBE ATOA YA MOYONI AKIREJEA CCM

    SHAKA ANG’AKA FAINI MIMBA ZA WANAFUNZI

    NI HISTORIA NYINGINE CCM

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM YATEUA MAKATIBU WA MIKOA NA WILAYA

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM ITAENDELEA KUWA CHAMA BORA, IMARA AFRIKA- SHAKA

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
  • Michezo
    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    PABLO AIPANIA KMC 

    PABLO AIPANIA KMC 

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
  • UMG
    • Home
    • About Us
    • Services
    • Shop
    • Contact Us
  • MAGAZETI
    • Uhuru wanawake
    • Mzalendo
    • Uhuru vijijini
    • Burudani
    • Uhuru kijani
  • UHURU FM
    • Ratiba
  • UHURU DIGITAL
    • Instagram
    • Facebook
    • Twitter
    • Youtube
  • Mwanzo
  • Siasa
    • All
    • Business
    MEMBE ATOA YA MOYONI AKIREJEA CCM

    MEMBE ATOA YA MOYONI AKIREJEA CCM

    SHAKA ANG’AKA FAINI MIMBA ZA WANAFUNZI

    NI HISTORIA NYINGINE CCM

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM YATEUA MAKATIBU WA MIKOA NA WILAYA

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAPOKEA TUZO CHAONGOZA KUWA NA WAFUASI WENGI MTANDAONI

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    CHONGOLO APIGILIA MSUMARI FEDHA ZA IMF

    SHAKA ATAJA SIRI CCM KUKUBALIKA

    CCM ITAENDELEA KUWA CHAMA BORA, IMARA AFRIKA- SHAKA

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
  • Michezo
    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    SIMBA, KAGERA NI KISASI, HESABU LEO

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    HAPATOSHI BURKINA FASO, SENEGAL  AFCON

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    MAYELE AIPA JEURI YANGA

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    NABI KUTUMIA MASTAA WAPYA MAPINDUZI CUP

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    SIMBA KIMATAIFA HATOKI MTU

    PABLO AIPANIA KMC 

    PABLO AIPANIA KMC 

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
No Result
View All Result
UHURU MEDIA GROUP
No Result
View All Result
Mwanzo Habari Kitaifa

WABUNGE WAJA JUU SAKATA LOLIONDO

>> WAIUNGA mkono serikali waisisitiza iendelee na msimamo wake kwa maslahi ya umma

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
June 21, 2022
in Habari Kitaifa
0 0
0
WABUNGE WAJA JUU SAKATA LOLIONDO

NAIBU Waziri wa Maliasili na Utalii, Mary Masanja (Mb) akitoa ufafanuzi wa hoja kuhusu Serikali kupandisha hadhi Maeneo ya Pori Tengefu ambayo hayana vijiji vya wananchi, Bungeni jijini Dodoma, Juni 20,2022.

0
SHARES
31
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

SERIKALI imesema hakuna vijiji vya wananchi katika eneo la Loliondo na Simanjiro, ambavyo vimetangazwa kuwa sehemu ya mapori ya akiba, huku wabunge wakikemea vitendo vya baadhi ya wanasiasa na wanaharakati kupotosha umma kuhusu wananchi wa Loliondo kwa kisingizio cha haki za binaadamu.

Imesisitiza eneo lote la ardhi ya Tanzania ni mali ya umma, hivyo maeneo ya mapori tengefu yaliyopandishwa hadhi kuwa mapori ya akiba kwa mujibu wa tangazo lililotolewa na Waziri wa Maliasili na Utalii, hayahusishi makazi ya watu.

Mjadala huo mkali uliibuka bungeni wakati wabunge wakichangia Hotuba ya Bajeti Kuu ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 baada ya Mbunge wa Simanjiro (CCM), Christopher Ole Sendeka, kudai jamii ya wafugaji inapitia katika taharuki kufuatia uamuzi wa serikali katika eneo la Ngorongoro na kupandisha hadhi baadhi ya mapori tengefu kuwa mapori ya akiba.

Alidai uamuzi huo wa Wizara ya Maliasili na Utalii kupandisha hadhi mapori hayo, unamaanisha Simanjiro itakuwa pori la akiba kwa asilimia 100.

Hata hivyo, alidai uamuzi huo unakinzana na matakwa ya sheria ambayo inaeleza hakuna ardhi ya kijiji itakayogeuzwa pori la akiba.

“Tangazo hilo linataka eneo lote la Simanjiro na eneo lote la Wilaya ya Longido kuwa pori la akiba. Kana kwamba hiyo haitoshi eneo la Ngorongoro lililokuwa Tarafa la Sare, nalo linamegwa kwa sura hii,” mbunge huyo alieleza katika mchango wake.

Wakati Ole Sendeka akiendelea na mchango wake, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Marry Masanja, alisimama kumuomba Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson, kumpatia nafasi ya kutoa taarifa kwa mchangiaji.

Naibu waziri huyo alipopewa nafasi alisema taarifa ya Waziri wa Maliasili na Utalii, iligusia maeneo ambayo hayatahusisha vijiji vya wananchi, hivyo maeneo yatakayopandishwa hadhi ni maeneo muhimu ya uhifadhi na hakuna vijiji vya wananchi.

Mara baada ya kutoa taarifa hiyo, Ole Sendeka alikataa kuipokea huku akitaka kutoa ufafanuzi zaidi jambo ambalo lilimlazimu Spika Tulia kumuhoji mbunge huyo kwa lengo la kutaka kupata ufafanuzi kuhusu madai hayo.

“Taarifa ya waziri inasema maeneo yaliyopandishwa hadhi hayana wananchi, mbunge anasema maeneo yana wananchi, upotoshajji upo katika maeneo gani? Hebu waziri tupe ufafanuzi na kama hakuna mwananchi, mchango wa Ole Sendeka nina mazungumzo nao,” aliagiza Dk. Tulia.

Akitoa ufafanuzi zaidi Naibu Waziri Marry alieleza: “Maeneo hayo yalikuwa mapori tengefu yana wawekezaji, tunapoona yana sifa ya kuhifadhiwa tunayapandisha hadhi ili wananchi wasiyasogelee.

“Tumeona haya maeneo yana hadhi na hayana wananchi. Tanzania ardhi ni ya umma, tunawagawa wananchi tunaposema haya maeneo ya kwangu. Asilimia 100 haya maeneo hawapo wananchi,” alisisitiza.

Baada ya kauli hiyo, spika alimtaka Ole Sendeka kusoma vifungu vya sheria vinavyosema mapori tengefu yamefutwa katika maeneo hayo, jambo ambalo mbunge huyo alinukuu baadhi ya vifungu ambavyo spika hakukubaliana navyo.

Kwa sababu hiyo Dk. Tulia alisema: “Maelekezo ya waziri mwenye sekta yanayosema wananchi wa Simanjiro na mapori tengefu wanaondoka, hakuna. Sasa haya maneno ya maeneo wanayokaa wamasai katika wilaya nne wataondoka yametoka wapi?. Waziri amesema maeneo hayo hakuna watu.

“Ukiambiwa unazikosea kanuni zetu kwa sababu umesema jambo ambalo halipo?. Kazi yangu hapa kusimamia kanuni, tukiendelea na mtindo huu mheshimiwa Ole Sendeka mimi nitataka uniletee ushahidi na waziri naye ataleta wa kwake halafu nitafanya maamuzi,” alisema.

Aliongeza: “Nilitaka nikurahisishie kama huna uhakika na hicho unachokisema tuliachie hapo. Kama unao uhakika nitataka uniletee ushahidi na waziri aniletee ushahidi na siyo ushahidi uliousema hapa. Mheshimiwa Ole Sendeka nakupa hiyo nafasi.”

Mara baada ya kupewa nafasi hiyo, Ole Sendeka alifuta maneno yake na kuendelea kuchangia mjadala huo wa bajeti kuu ya serikali.

Kwa upande wake, Mbunge wa Viti Maalumu (CHADEMA) Jesca Kishoa, alisema ripoti ya utafiti ya Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI) ya mwaka 2020 inaeleza idadi ya watu eneo la Ngorongoro imeongezeka mara tano zaidi ya miaka ya 1970.

Alisema katika eneo hilo idadi ya mifugo imeongezeka kutoka 19,100 hadi 805,000, ambapo mwaka 1970 kila mtu mmoja alikuwa akiishi wastani wa kilomita moja za mraba, lakini mwaka 2019 uwiano ulifikia mtu mmoja akiishi kilomita za mraba 0.084 sawa na watu 11 kukaa katika kilomita moja ya mraba, bila kujumuisha eneo la kuishi wanyama.

“Wanasiasa na wanaharakati waache kupotosha wananchi kupitia kiraka cha haki za binadamu, ninaungana na Rais Samia Suluhu Hassan kulinda urithi wa Tanzania, ninaungana na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa katika kulinda urithi wa taifa, ninaungana na wananchi kulinda urithi wa taifa,” alisema.

Alisisitiza: “Mkuu wa nchi asirudi nyuma, vizazi na vizazi vitamkumbuka. Tunahitaji keki hiyo ya taifa inufaishe vizazi na vizazi, tuambieni ukweli ni wapi Afrika

Mashariki kilikowahi kufanyika kilichofanyika pale Handeni? Unapelekwa eneo unajengewa nyumba, hospitali, shule na zahanati.

“Kuna taarifa wapo wabunge wanatetea haya kwa maslahi ya mashemeji zao humu. Kusema kuwahamisha ni makosa kwa sababu wameyazoea tunajenga kitu kibaya, endapo wengine wakihamishwa ili kujenga miundombinu watakataa wakisema mbona Ngorongoro walikataa kwa sababu maeneo yao wameyazoea,” alisisitiza.

Mbunge huyo alishauri hatua rafiki zifanyike wakati wa kuwahamisha wananchi katika eneo hilo na kuainisha idadi ya wananchi wanaohitajika kubaki.

Pia, alisema ni muhimu eneo ambalo wananchi hao wanapelekwa wapelekwe madaktari na walimu wa kutosha.

Mbunge wa Mvumi (CCM), Livingstone Lusinde, alisema kwa matendo yasiyokuwa ya kizalendo yanayoendelea, ipo siku huruma ya Rais Samia itaondoka.

Lusinde alisema hakuna katika Tanzania watu waliohama vizuri kama wanaohamishwa kutoka Ngorongoro.

Alisema katika miaka iliyopita wakati wafugaji wanahamishwa kwenda mikoa ya kusini wengine mifugo yao ilikufa njiani, lakini wafugaji kutoka Ngorongoro wamehamishwa kwa kupatiwa maeneo yenye ukubwa wa ekari tatu.

“Wamepewa ardhi ya ekari tatu, tumsaidie Rais kuwaelimisha watu umuhimu wa maeneo haya, sisi tusiwe vikwazo,” alisisitiza.

HOJA NYWELE BANDIA

Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Hawa Mwaifuge, alisema kabla ya serikali kufanya uamuzi wa kupandisha kodi ya nywele bandia, ifanye utafiti kubaini idadi ya viwanda nchini vinavyozalisha nywele hizo na kwa kiwango kipi cha ubora.

Alisema uamuzi wa kupandisha kodi katika nywele hizo unaweza kuathiri maendeleo ya viwanda vya nywele nchini na kusababisha kufa badala ya kuimarika.

“Biasharayanyweleinafanywanakinamama ambao wanalipa kodi ya serikali, hawajawahi kukwepa kodi. Sisi katika viwanda vyetu tupo tayari kutengeneza wigi (nywele bandia) zenye ubora?. Tuwaache kina dada wafanye biashara, wanaleta nywele nzuri. Hii ni sekta muhimu tuache kodi kama ilivyo ili wanawake wafanye biashara vizuri,” alieleza.

Akizungumzia pendekezo la serikali kuchukua asilimia tano kati ya 10 inayotengwa na halmashauri kwa lengo la kuboresha miundombinu ya wafanyabiashara wadogo, alisema uamuzi huo utaathiri wajasiriamali.

Alisema hata asilimia 10 ya mapato ya halmashauri kutengwa kuwawezesha wajasiriamali kwa kuwapatia mikopo bado haitoshi.

“Nilitamani serikali ije na pendekezo la kuongeza asilimia 15 badala ya kupunguza asilimia 10. Tafuteni utaratibu mzuri kuhakikisha wajasiriamali wanapata maeneo yao lakini siyo kuchukua hela hizo,” alieleza.

MISAMAHA YA KODI

Mbunge wa Kinondoni (CCM) Abbas Tarimba, aliishauri serikali kuimarisha sekta zisizokuwa rasmi ili ziimarike kuwa sekta rasmi zilipe kodi kukuza uchumi wa nchi.

Pia, alisema kuna umuhimu serikali kutoa misamaha ya kodi katika maeneo yenye kumgusa mwananchi moja kwa moja na siyo maeneo ambayo hayaleti tija kwa wananchi.

“Tuliweka msamaha wa kodi kwenye simu janja lakini ziliwanufaisha wafanyabiashara, tukaweka msamaha kwenye taulo za kike zikawanufaisha wafanyabiashara. Tunaweka msamaha katika mitungi ya gesi badala ya kuweka msamaha katika gesi ambayo inawasaidia wananchi,” alieleza Tarimba.

Na MUSSA YUSUPH, Dodoma

Abdurahman Jumanne

Abdurahman Jumanne

Stay Connected test

  • 114 Follower
  • 172k Subscriber
  • 23.6k Follower
  • 99 Subscriber
  • Trending
  • Comments
  • Latest
MADAKTARI WAELEZEA JINSI YA KUZUIA MIMBA ISIHARIBIKE

MADAKTARI WAELEZEA JINSI YA KUZUIA MIMBA ISIHARIBIKE

July 9, 2021
TABWA YAMSIFU SAMIA KUWAPA FURSA WANAWAKE

TABWA YAMSIFU SAMIA KUWAPA FURSA WANAWAKE

July 9, 2021
BEI MPYA YA MBAAZI, KUNDE YAWAPANDISHA MZUKA WAKULIMA

BEI MPYA YA MBAAZI, KUNDE YAWAPANDISHA MZUKA WAKULIMA

August 9, 2021
MBUNGE LINDI ATAKA VIJANA WAJISHUGHULISHE

MBUNGE LINDI ATAKA VIJANA WAJISHUGHULISHE

July 8, 2021
NDUGU MATATANI KUMSHAMBULIA, KUMJERUHI MWENZAO KISA NG’OMBE

NDUGU MATATANI KUMSHAMBULIA, KUMJERUHI MWENZAO KISA NG’OMBE

0
WAHANDISI WA HALMASHAURI WAMEKUA WAKIIKOSEA SERIKALI KWAKUTOA TAARIFA ZA UONGO

WAHANDISI WA HALMASHAURI WAMEKUA WAKIIKOSEA SERIKALI KWAKUTOA TAARIFA ZA UONGO

0

OFISA ELIMU, MHANDISI, MKUU WA SHULE WAKALIA ‘KUTI KAVU’

0
STENDI YA ZAMANI UBUNGO  KUJENGWA DEPO MABASI MWENDOKASI

STENDI YA ZAMANI UBUNGO KUJENGWA DEPO MABASI MWENDOKASI

0
MIAKA 30 YA VYAMA VINGI: CHANGAMOTO NA MUSTAKABALI KUSONGA MBELE

MIAKA 30 YA VYAMA VINGI: CHANGAMOTO NA MUSTAKABALI KUSONGA MBELE

July 1, 2022
WAWILI WADAKWA DAR TUHUMA ZA BIASHARA YA NGONO MTANDAONI

WAWILI WADAKWA DAR TUHUMA ZA BIASHARA YA NGONO MTANDAONI

June 28, 2022
WAJUE WATIKISA NYAVU BORA 2021/2022

WAJUE WATIKISA NYAVU BORA 2021/2022

June 28, 2022
ATOZWA FAINI 100,000 KISA KUIBA PUNDA WA BABA YAKE

ATOZWA FAINI 100,000 KISA KUIBA PUNDA WA BABA YAKE

June 28, 2022

Recent News

MIAKA 30 YA VYAMA VINGI: CHANGAMOTO NA MUSTAKABALI KUSONGA MBELE

MIAKA 30 YA VYAMA VINGI: CHANGAMOTO NA MUSTAKABALI KUSONGA MBELE

July 1, 2022
WAWILI WADAKWA DAR TUHUMA ZA BIASHARA YA NGONO MTANDAONI

WAWILI WADAKWA DAR TUHUMA ZA BIASHARA YA NGONO MTANDAONI

June 28, 2022
WAJUE WATIKISA NYAVU BORA 2021/2022

WAJUE WATIKISA NYAVU BORA 2021/2022

June 28, 2022
ATOZWA FAINI 100,000 KISA KUIBA PUNDA WA BABA YAKE

ATOZWA FAINI 100,000 KISA KUIBA PUNDA WA BABA YAKE

June 28, 2022
Instagram Youtube Twitter VK Facebook

We are a diverse team of experts, innovative thinkers, creative designers, writers, innovators, strategists, pyschologists, comunictaors and web developers. UMG is extremely passionate about growing clients’ businesses, helping them achieve their goals and making a difference by raising the creative and communications industry standards in Tanzania.

Follow Us

Browse by Category

  • 2021
  • Afya Makala
  • BURUDANI
  • Business
  • GAZETI LA BURUDANI
  • GAZETI LA UHURU
  • GAZETI LA UHURU MACHI 17
  • HABARI KIMATAIFA
  • Habari Kitaifa
  • Habari Picha
  • KIMATAIFA
  • MAKALA
  • MAKALA AFYA
  • MAKALA-BURUDANI
  • MICHEZO
  • MICHEZO KIMATAIFA
  • MICHEZO KITAIFA
  • MICHEZO-MAKALA
  • MICHEZO-MASUMBWI
  • MITINDO
  • RIWAYA
  • SIASA
  • Uncategorized

Recent News

MIAKA 30 YA VYAMA VINGI: CHANGAMOTO NA MUSTAKABALI KUSONGA MBELE

MIAKA 30 YA VYAMA VINGI: CHANGAMOTO NA MUSTAKABALI KUSONGA MBELE

July 1, 2022
WAWILI WADAKWA DAR TUHUMA ZA BIASHARA YA NGONO MTANDAONI

WAWILI WADAKWA DAR TUHUMA ZA BIASHARA YA NGONO MTANDAONI

June 28, 2022

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

No Result
View All Result

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In